MENU

SEARCH HERE/ TAFUTA HAPA

Saturday, October 23, 2021

UFAAFU WA ANWANI CHECHE ZA MOTO na KAKA BOLLO

 UFAAFU WA ANWANI CHECHE ZA MOTO-MWONGOZO WA CHECHE ZA MOTO

Maana ya cheche-Cheche ni vijisehemu vya kitu chenye mwangaza, vinavyotoa mwanga au mwangaza. Maana ya cheche za moto- Vijisehemu vya moto vinvyoweza kusababisha moto vikiruka na kutua katika mazingira yanayowezakusababisha/ kukuza moto. Katika riwaya ya Cheche za Moto, anwani hii inarejelea vitendo vinavyohatarisha maisha ya wananchi wa kawaida, kuwaletea maumivu au hata vifo. Cheche za moto katika riwaya hii zinatolewa na kiongozi Osman Jumbe, Askari Jeshi, Polisi, kachero wa Osman Jumbe na vyombo vingine vya Dola.

Anwani hii inaifaa riwaya hii kwa sababu inadokeza kwa undani mifano kadhaa ya cheche za moto kama ifuatavyo:

1.   Askari wanampiga Benta risasi kwake nyumbani na kutoweka na mumewe uk 14.

2.   Askari wanambaka mkewe Mule na wengine jumajiana na Mule kishoga uk. 5, 6

3.   Mafuvu ya vichwa vinajazwa kule The Red Valley wakati wa utawala wa Osman Jumbe uk. 5

4.   Askari anamfyatua Mwanakombo risari na kumuua uk. 6/uk. 9

5.   Askari wanawa piga Mule, mkewe na Rita wanapowavamia uk. 3, 5

6.   Wasichana na wavulana wadogo kupigwa risasi uk. 23

7.   Vita kati ya askari Ali na askari jeshi watatu uk. 20

8.   Polisi anamuua kijana kwa kugombania mwanamke vilabuni uk. 25

9.   Osman Jumbe anawaambia Wahindi wa Malanga waondoke warudi kwao uk. 27

10. Masaba anatolewa kwake na askari baaba ya kuambiwa aiage familia yake uk. 35/37    

          KUNA MIFANO MINGINE ZAIDI YA HAMSINI KATIKA MWONGOZO WETU

MWONGOZO HUU PIA UMESHEHENI YAFUATAYO:

1. Wahusika na sifa zao

2. Dhamira ya mwandishi

3. Maudhui na maelezo yao

4. Mbinu za uandishi na mifano yao

5. Maswali ya kudurusu

JIPATIE NAKALA YA MWONGOZO WA CHECHE ZA MOTO 

            NUNUA MWONGOZO WA RIWAYA YA CHECHE ZA MOTO KUTOKA KWETU KWA SHILINGI 500 PEKEE

            BONYEZA HAPA ILI KUNUNUA MWONGOZO-TUMA SHILINGI MIA TANO

PIA TUNAWAPA MAELEKEZO WANAFUNZI KATIKA RIWAYA YA CHECHE ZA MOTO

WASILIANA NASI KWA NAMBARI 0702371829 KWA MAELEZO ZAIDI

ULIZA SWALI AU TOA MAONI KATIKA SEHEMU YA MAONI HAPA CHINIπŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡


Saturday, August 21, 2021

UCHAMBUZI NA MWONGOZO WA RIWAYA YA CHECHE ZA MOTO na KAKA BOLLO

 UCHAMBUZI WA CHECHE ZA MOTO

BONYEZA HAPA KUNUNUA MWONGOZO WA CHECHE ZA MOTO KWA  SHILINGI 500

 Uchambuzi wa Riwaya ya Cheche za Moto unashugulikia maswala makuu kama vile:

  •  Mtiririko wa vitushi na ploti, 
  • Wahusika na sifa zao, 
  • Dhamira ya mwandishi, 
  • Maudhui
  • Na maswali ya kutarajiwa katika mitihani mbalimbali itakayi tahini riwaya hii.

Uchambuzi huo umeng'oa nanga na umeshika kasi. Baada ya mchakato mzima, tutachapisha makala hayo ya uchambuzi ambayo yatawafaa wakufunzi na wanafunzi kwa pamoja.

Kampuni hii itauza makala hayo kwa shilingi mia tano kwa kila nakala. Vilevile, tutachapisha baadhi ya sehemu za makala hayo humu ili kuwafaidi wale wanaotumia wavuti na simu za mkono kama njia ya kujielimisha.

TUNAWAKUMBUSHA wasomaji wetu kwamba tutachapisha video za uchambuzi wa makala haya katika YouTube kwa wale wanaoelimika bora kwa kusikiliza na kutazama. Kwa hivyo tunawakumbusha wasomaji wetu ku-SUBSCRIBE channel yetu ili kupata ujumbe kuhusu makala/video hizo tunapoyaweka au kuyapakia humo. 

BONYEZA HAPA ILI KUSUBSCRIBE

Kuuliza swali, andika swali lako kwenye sehemu ya "comment" hapa chini.πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡


Wednesday, June 9, 2021

VITABU VIPYA VYA FASIHI ANDISHI VYA SHULE ZA UPILI 2021

VITABU VIPYA VYA FASIHI ANDISHI VYA SHULE ZA UPILI 2021

Subscribe to our Youtube Channel for updates on CHECHE ZA MOTO analysis videos and other updates
Click here> YouTube


Wizara ya Elimu imeidhinisha vitabu vipya vya fasihi andishi vitakavyosomwa, kuchambuliwa na kutahiniwa katika shule za upili kote nchini.

CHECHE ZA MOTO iliyoandikwa na John Habwe na kuchapishwa na Jomo Kenyatta Foundation (JKF) ndiyo riwaya ambayo itachukua nafasi ya riwaya ya Chozi la Heri ya Asumpta K. Matei.

Hadithi fupi, MAPAMBAZUKO YA MACHWEO iliyochapishwa na kampuni ya ushapishaji ya Mountain Top ndiyo itachukua nafasi ya Tumbo Lisiloshiba na hadithi nyingine iliyohaririwa na Alifa Chokocho na Dumu Kayanda.

Wizara ya elimu imeidhinisha vitabu hivi baada ya miaka minne ya kutahiniwa kwa Chozi la Heri na Tumbo Lisiloshiba. 

Wakufunzi wameelezea matarajio makuu kwamba Cheche za Moto huenda ikawa nyepesi kwa wanafunzi kuelewa hasa kwa kuzingatia mtitiriko wa vitushi na idadi ya wahusika. Baadhi ya walimu wamedokeza kwamba riwaya inayoondoka imekuwa changamoto kwao na kwa wanafunzi kwa sababu imeshishirikisha wahusika chungu nzima. Vilevile, walimu hao wameeleza kwamba riwaya Chozi la Heri imekuwa na uchangamano mwingi katika muundo wake.

Kwa upande mwingine, wanafunzi waliohojiwa na Homeschool Kenya wamepongeza watunzi mbalimbali wa hadithi katika diwani ya Tumbo Lisiloshiba. Wanafunzi hao wamedokeza kwamba hadithi hizo mbali na kuburudisha, zimesheheni ujumbe muhimu kwa wanafunzi wote. Nilipowauliza kuhusu changamoto walizokumbana nazo katika usomaji wao wa Tumbo Lisiloshiba, wanafunzi hao walisisitiza kwamba hadithi hizo zimekuwa nyepesi kuelewa.

Tunashughulikia uchambuzi wa Cheche za Moto na Mapambazuko ya Machweo na baada ya siku chache tutachapisha makala hayo humu kwenye blogu kwa manufaa yetu sote. Ahsanteni.


Wasiliana nasi Kupitia WhatsApp. 

Kwa makala mengine gusa yafuatayo:


 

Tuesday, June 8, 2021

VITABU VIPYA VYA FASIHI ANDISHI VYA SHULE ZA UPILI 2021

 

VITABU VIPYA VYA FASIHI ANDISHI VYA SHULE ZA UPILI 2021

Subscribe to our Youtube Channel for updates on CHECHE ZA MOTO analysis videos and other updates
Click here> YouTube
Wizara ya Elimu imeidhinisha vitabu vipya vya fasihi andishi vitakavyosomwa, kuchambuliwa na kutahiniwa katika shule za upili kote nchini.

CHECHE ZA MOTO iliyoandikwa na John Habwe na kuchapishwa na Jomo Kenyatta Foundation (JKF) ndiyo riwaya ambayo itachukua nafasi ya riwaya ya Chozi la Heri ya Asumpta K. Matei.

Hadithi fupi, MAPAMBAZUKO YA MACHWEO iliyochapishwa na kampuni ya ushapishaji ya Mountain Top ndiyo itachukua nafasi ya Tumbo Lisiloshiba na hadithi nyingine iliyohaririwa na Alifa Chokocho na Dumu Kayanda.

Wizara ya elimu imeidhinisha vitabu hivi baada ya miaka minne ya kutahiniwa kwa Chozi la Heri na Tumbo Lisiloshiba. 

Wakufunzi wameelezea matarajio makuu kwamba Cheche za Moto huenda ikawa nyepesi kwa wanafunzi kuelewa hasa kwa kuzingatia mtitiriko wa vitushi na idadi ya wahusika. Baadhi ya walimu wamedokeza kwamba riwaya inayoondoka imekuwa changamoto kwao na kwa wanafunzi kwa sababu imeshishirikisha wahusika chungu nzima. Vilevile, walimu hao wameeleza kwamba riwaya Chozi la Heri imekuwa na uchangamano mwingi katika muundo wake.

Kwa upande mwingine, wanafunzi waliohojiwa na Homeschool Kenya wamepongeza watunzi mbalimbali wa hadithi katika diwani ya Tumbo Lisiloshiba. Wanafunzi hao wamedokeza kwamba hadithi hizo mbali na kuburudisha, zimesheheni ujumbe muhimu kwa wanafunzi wote. Nilipowauliza kuhusu changamoto walizokumbana nazo katika usomaji wao wa Tumbo Lisiloshiba, wanafunzi hao walisisitiza kwamba hadithi hizo zimekuwa nyepesi kuelewa.

Tunashughulikia uchambuzi wa Cheche za Moto na Mapambazuko ya Machweo na baada ya siku chache tutachapisha makala hayo humu kwenye blogu kwa manufaa yetu sote. Ahsanteni.

πŸ’«
Wasiliana nasi Kupitia WhatsApp. 

Kwa makala mengine gusa yafuatayo:

Wednesday, February 24, 2021

TAMTHILIA YA KIGOGO: SUMU YA NYOKA

TAMTHILIA YA KIGOGO: ATHARI YA SUMU YA NYOKA SAGAMOYO

#Wasiliana nasi. Bonyeza hapa

 


Athari za sumu ya nyoka

1)    Vifo- Ngao junior

2)    Watu wanageuka vipofu-Mngweni kwa mama pima

3)    Ukengeushi mf. Ngurumo

4)    Kuanguka chini ovyo ovyo na kugaragara-walevi mangweni

5)    Wanafunzi katika shule ya Majoka wamegeuka vichwa  maji- ni makabeji

6)    Walevi hawafahamu athari za ulevi.

7)    Hawaoni athari ya soko kufungwa- Chapakazi

8)    Kupotosha vijana ( gume gume)

9)    Kupotoka kwa maadili

10)Kuvunjika kwa ndoa

 #Nunua Mitihani@Kshs. 100

11)Waathiriwa wanatumiwa na viongozi kutekeleza maovu mf. Ngurumo kumvinja Tunu muundi.

12)Utepetevu ( uzembe) wanashinda ulevini na kupoteza muda.

13)Kuwaunga mkono viongozi  wasiowajibika baada ya kupewa vipeni. ( vibaraka) kama vile Ngurumo

14)Kutumia lugha chafu/ matusi mf Ngurumo kumtusi Tunu.

15)Kukosa wachumba/ ukapera mf Ngurumo

16)Dharau-Ngurumo kumdharau Tunu na kumwimbia wimbo wa Kuolewa-wa Daudi Kabaka

17)Kufuja pesa

18)Kutofuata maagizo – Chopi hakufuata maagizo ya kumuua Tanu.

 #TAZAMA MADA YA ZIADA KWENYE YOUTUBE

1. CHOZI LA HERI

2. TUMBO LISILOSHIBA

3. KIGOGO

4. FASIHI SIMULIZI

TOA MAONI HAPA KWENYE SEHEMU YA MAONIπŸ‘‡

Sunday, February 14, 2021

UJUMBE WA DHARURA KWA WALIMU WOTE

 

UJUMBE WA DHARURA KWA WAKUFUNZI WOTE

Ni mwaka mpya ambapo mchakato wa mafunzo umeanzishwa tena rasmi baada ya kusitishwa mwaka uliopita kutokana na janga la tandavu la Korona. Katika wiki chache ambazo tumekuwa tukitimiza malengo yetu kwa kuwahudumia wanafunzi kwa njia ya mafunzo, tumeshuhudia ukatili miongoni mwa mwao katika baadhi ya shule humu nchini. Ukatili huu umehatarishs maisha ya walimu katika shule husika. Ni muhimu kutambua kwamba usalama wako ni muhimu sana, kwa hivyo huna budi kuusisitizia. Zifuatazo ni njia ambazo kulingana nami, zitaweza kutusaidia kuepuka ukatili na udhalimu wa wanafunzi.

Zingatia jukumu kuu ambalo uliajiriwa kutekeleza. Iwapo umesahau, rejelea barua yako ya kazi kutoka kwa tume ya kuajiri walimu. Kila mara hakikisha kwamba umetimiza jukumula kutimiza jukumu lako, na kwa kiwango kinashoridhisha matarajio yako, ya mwajiri na ya jamii. Kukosa kutimiza jukumu huweza ukazua uhasama wa wanafunzi dhidi yako, jambo ambalo huenda likatishia usalama wako. Wanafunzi wa sasa japo wamepungukiwa na motisha ya kujituma masomoni kutokana na athari za mienendo na maisha ya kijamii, wanatambua wakati ambapo wanapokea huduma bora kutoka kwa Mwalimu na wakati ambapo wanapokea bora huduma.

Je, sheria inakupa nguvu za kumwadhibu mwanafunzi? La. Ni muhimu kila mkufunzi kufahamu fika kwamba sote (walimu na wanafunzi) tuko katika karne ambayo mawasiliano hayana vizingiti. Yanapenya na kupokelewa na kila rika. Kwa hivyo tusipuuze ukweli kwamba wanafunzi hawa wanafahamu kwamba adhabu ni kinyume cha sharia. Wakati mwingine unaweza ukagundua kuwa mwanafunzi anapuuza hitaji lako la kumwadhibu akijua kwamba unakiuka sharia.Wewe kama mkufunzi huenda ukakerwa na jambo hili. Kabla hasira hazijakutawala, hebu jiulize iwapo kumpa mwanafunzi adhabu nimoja kati ka majukumu uliyokabidhiwa na tume.

Kupitia masomo ya saikolojia kwenye vyuo mbalimbali tulikosomea ualimu, kila mwalimu aliyekuwa makini kwa masomo hayo bila shaka anapaswa kuwa na uwezo wa kutambua ama kung’amua fikra za wanafunzi kutokana na jinsi wanavyozungumza ama kutenda mambo yao. Iwapo umegundua kisicho kawaida katika tabia na mienendo ya mwanafunzi, kinachoweza kuhatarisha maisha yako, kumbuka kuwa ni muhimu kutahadhari kabla ya hatari. Kwa mfano, ukimwona mwanafunzi na kifaa kisichohitajika shuleni kama kisu, chukua hatua kwa kufuata mchakato unaofaa ili apikonywe kifaa hicho.

Mwanafunzi anapojeruhiwa ama kwa behati mbaya, anapokufa mikonomi mwa Mwalimu, magari makubwa makubwa huja skulini kumchukulia hatua mkufunzi husika. Mwalimu anapopitia yayo hayo mikononi mwa wanafunzi, ni muhali kuona wakuu wakija kuwachukulia wanafunzi hatua. Hili ni thibitisho tosha kwamba wewe kama Mwalimu, kila mja anaamini kuwa unauwezo wa kujilinda na kujihakikishia usalama wako. Kwa hiyo tambua kwamba usalama wako unakutegemea wewe mwenyewe.

Kwa jumla, wazo langu kihusu usalama wa Mwalimu ni kwamba usalama huo unamtegemea Mwalimu mwnyewe. Kwanza, epuka matendo ambayo huenda yakazua uhasama kati yako na wanagenzi. Pili, fahamu fika jukumu lako na ulitimize ipasayvo. Tatu, chunguza na utambue tabia hasi miongoni mwa wanafunzi ambazo huenda zikaangamiza usalama wako, kisha chukua hatua kuzikomesha. Mwisho, unauwezo wa kujihakikishia usalama na kujilinda. Jilinde.