MENU

SEARCH HERE/ TAFUTA HAPA

Tuesday, July 22, 2025

SHAMIRISHO KATIKA KISWAHILI (KIPOZI, KITONNDO, NA ALA)

 

SHAMIRISHO KATIKA KISWAHILI

SHAMIRISHO KATIKA KISWAHILI

MAANA YA SHAMIRISHO:

Shamirisho ni neno ambalo huashiria nomino inayopokea kitendo (kitendwa/mtendwa), nonimo inayofaidika kutokana na kitendo (kitendewa/mtendewa), na kifaa kinachotumika katika kitendo (ala), katika sentensi.

AINA ZA SHAMIRISHO

1. Shamirisho Kipozi/ Yambwa Tendwa

2. Shamirisho Kitondo/ Yambwa Tendewa/yambiwa

3. Shamirisho Ala/ Kitumizi

------------------------------------------------------------------------------

1. SHAMIRISHO KIPOZI

Pia huitwa yambwa tendwa (Direct object).
Ni nomino anayopokea athari ya kitendo moja kwa moja.
Mara nyingi hipatikana katika sentensi zilizoandikwa katika kauli ya kutenda, japo huwezakupatikana katika sentensi zilizoandikwa katika kauli zingine.

Mifano

  1. Wizara ya elimu inarekebisha mtaala. (mtaala-shamirisho kipozi)
  2. Mkulima analima shamba.  (shamba-shamirisho kipozi)
  3. Mgonjwa aliletewa chai kwa chupa na Swaleh. 
  4. Kitabu cha mwanafunzi kimepotezwa na mtoto.
  5. Kipenga cha mkufunzi kitanunuliwa wiki ijayo na mwalimu mkuu.
----------------------------------------------------------------------
----------------------------------------------------------------------
2. SHAMIRISHO KITONDO
Pia huitwa yambwa tendewa au yambiwa (Indirect Object).
Ni nomino ambayo huathiriwa na kitendo kwa njia isiyo ya moja kwa moja.
Huathiriwa na kitendo kinacho tendwa kwa shamirisho kipozi.
Hupatikana katika sentensi zilizoandikwa katika kauli ya kitendea/ kutendewa.

Mifano
  1. Mzazi alimnunulia mwanawe baiskeli kwa kupita mtihani.
  2. Kaka atamfyekea babu yangu shamba baada ya kutoa mahindi.
  3. Nina alimpikia mgonjwa chakula chenye ladha tamu.
  4. Walimu waliwekewa runinga kwanye afisi yao.
  5. Mwanasiasa alipigiwa kura na kushinda uchaguzi mdogo wa mkoa.
----------------------------------------------------------------------
3. SHAMIRISHO ALA/ KITUMIZI
Ni nomino ambayo hurejelea kifaa kinachotumiwa kitekeleza kitendo fulani.
Huwakilishwa na vielezi vya namna ala.
KUMBUKA: "kwa" si sehemu ya shamirisho ala.

Mifano
  1. Kaka alilima shamba lake kwa jembe jipya.
  2. Mpishi alikata vitunguu na nyanya kwa kisu.
  3. Mwalimu alisahihisha vitabu vya wanafunzi kwa kalamu.
  4. Juma alisafiri ughaibuni kwa ndege.
  5. Viwanja vilinunuliwa kwa pesa
  6. Mkongwe atajengewa nyumba ya mbao.
----------------------------------------------------------------------
----------------------------------------------------------------------
SHUKRAN KWA USOMAJI WAKO 🙏👍😎

UNA SWALI KUHUSU SHAMIRISHO KIPOZI, KITONDO, AMA SHAMIRISHO ALA?
ULIZA HAPA CHINI 👇👇


Thursday, July 17, 2025

SHAMIRISHO KIPOZI, KITONDO, NA ALA

SHAMIRISHO KATIKA KISWAHILI

SHAMIRISHO KATIKA KISWAHILI

MAANA YA SHAMIRISHO:

Shamirisho ni neno ambalo huashiria nomino inayopokea kitendo (kitendwa/mtendwa), nonimo inayofaidika kutokana na kitendo (kitendewa/mtendewa), na kifaa kinachotumika katika kitendo (ala), katika sentensi.

AINA ZA SHAMIRISHO

1. Shamirisho Kipozi/ Yambwa Tendwa

2. Shamirisho Kitondo/ Yambwa Tendewa/yambiwa

3. Shamirisho Ala/ Kitumizi

------------------------------------------------------------------------------

1. SHAMIRISHO KIPOZI

Pia huitwa yambwa tendwa (Direct object).
Ni nomino anayopokea athari ya kitendo moja kwa moja.
Mara nyingi hipatikana katika sentensi zilizoandikwa katika kauli ya kutenda, japo huwezakupatikana katika sentensi zilizoandikwa katika kauli zingine.

Mifano

  1. Wizara ya elimu inarekebisha mtaala. (mtaala-shamirisho kipozi)
  2. Mkulima analima shamba.  (shamba-shamirisho kipozi)
  3. Mgonjwa aliletewa chai kwa chupa na Swaleh. 
  4. Kitabu cha mwanafunzi kimepotezwa na mtoto.
  5. Kipenga cha mkufunzi kitanunuliwa wiki ijayo na mwalimu mkuu.
----------------------------------------------------------------------
----------------------------------------------------------------------
2. SHAMIRISHO KITONDO
Pia huitwa yambwa tendewa au yambiwa (Indirect Object).
Ni nomino ambayo huathiriwa na kitendo kwa njia isiyo ya moja kwa moja.
Huathiriwa na kitendo kinacho tendwa kwa shamirisho kipozi.
Hupatikana katika sentensi zilizoandikwa katika kauli ya kitendea/ kutendewa.

Mifano
  1. Mzazi alimnunulia mwanawe baiskeli kwa kupita mtihani.
  2. Kaka atamfyekea babu yangu shamba baada ya kutoa mahindi.
  3. Nina alimpikia mgonjwa chakula chenye ladha tamu.
  4. Walimu waliwekewa runinga kwanye afisi yao.
  5. Mwanasiasa alipigiwa kura na kushinda uchaguzi mdogo wa mkoa.
----------------------------------------------------------------------
3. SHAMIRISHO ALA/ KITUMIZI
Ni nomino ambayo hurejelea kifaa kinachotumiwa kitekeleza kitendo fulani.
Huwakilishwa na vielezi vya namna ala.
KUMBUKA: "kwa" si sehemu ya shamirisho ala.

Mifano
  1. Kaka alilima shamba lake kwa jembe jipya.
  2. Mpishi alikata vitunguu na nyanya kwa kisu.
  3. Mwalimu alisahihisha vitabu vya wanafunzi kwa kalamu.
  4. Juma alisafiri ughaibuni kwa ndege.
  5. Viwanja vilinunuliwa kwa pesa
  6. Mkongwe atajengewa nyumba ya mbao.
----------------------------------------------------------------------
----------------------------------------------------------------------
SHUKRAN KWA USOMAJI WAKO 🙏👍😎

UNA SWALI KUHUSU SHAMIRISHO KIPOZI, KITONDO, AMA SHAMIRISHO ALA?
ULIZA HAPA CHINI 👇👇