MENU

SEARCH HERE/ TAFUTA HAPA

Sunday, May 31, 2020

'O' NA 'AMBA' REJESHI: MASWALI NA MAJIBU


 “O” NA “AMBA” REJESHI: MASWALI NA MAJIBU


MAKUENI
Iandike sentensi ifuatayo kwa kutumia ‘O’ rejeshi. (alama 2 )
Kijana ambaye hutumbuiza watu ametuzwa.
JIBU: Kijana atambuizaye watu ametuzwa.

HOMABAY

Unganisha sentensi hizi kwa kutumia kirejeshi cha kati. (alama 2)
(i) Kalamu imeibwa
(ii) Kalamu ni yangu
JIBU: Kalamu iliyoibwa ni yangu

RABAI

Andika sentensi hii upya ukitumia ‘o’ rejeshi tamati.
Zimwi ambalo humla mtu ni lile ambalo linaogopewa. (alama 2)
JIBU: Zimwi lilalo mtu ni lile liogopewalo

KIHARU

Tumia kirejeshi “O” tamati katika sentensi ifuatayo. (alama 1)
Kijana ambaye anapendendeza ni yule ambaye hutia bidii.
JIBU: Kijana apendezaye ni yule atiaye bidii.

NANDI YA KATI

Tunga sentensi ukitumia kirejeshi tamati. (alama 1)
JIBU: Asomaye kwa bidii hufaulu. (alama 1)
(sentensi ionyeshe kuwa kirejeshi tamati huonyesha mazoea)

NANDI KASKAZINI

Tumia ‘amba’ rejeshi katika sentensi ifuatayo: (alama 2)
Mchezaji ninayempenda ni Messi.
JIBU: Mchezaji ambaye ninampenda ni Messi.

NANDI KUSINI –TINDIRET

Kanusha bila kutumia ‘amba’ (alama 2)
Nitamtuza mwanafunzi ambaye ni nadhifu.
JIBU:Sitamtuza mwanafunzi asiye nadhifu.

ELDORET MAGHARIBI

Andika upya bila ya kutumia ‘amba’: (alama 1)
Mtoto ambaye alianguka shimoni ametibiwa.
JIBU: Mtoto aliyeanguka shimoni ametibiwa.

KERICHO

Tumia kirejeshi ‘O’ tamati katika sentesi ifuatayo : (al.2)
Kalamu ambayo alinunua ni ile ambayo anaipenda.
JIBU: Kalamu ainunuayo ni ile aipendayo

NANDI KATI

Tumia ‘amba’ katika sentensi ifuatayo. (alama 1)
Wanafunzi wapitao mtihani husherehekea.
JIBU: Wanafunzi ambao hupita mtihani husherehekea.

KEIYO

Sunday, May 24, 2020

WAHUSIKA KATIKA TUMBO LISILOSHIBA

WAHUSIKA KATIKA TUMBO LISILOSHIBA


Katika fasihi, mhusika ni kiumbe aliyefasiriwa au kubuniwa na mtunzi, anayemwiga na kufanana na kiumbe halisi duniani kwa kiasi Fulani. Kuna aina mbalimbali za wahusika kama vile:

a)    Mhusika mkuu

Huyu ni mhusika ambaye anajitokeza katika hadithi kwa kiasi kikubwa zaidi kuliko wahusika wengine. Huweza kujitokeza kuanzia mwanzo hadi mwisho wa hadithi.

b)    Wahusika wadogo/ wasaidizi

Hawa ni wahusika ambao hutangamana na mhusika mkuu na kumsaidia kuibua dhamira na maudhui katika hadithi. Wahusika hawa hujitokeza kwa kiasi kidogo tu kwenya hadithi na kisha kupotea.

Diwani ya Tumbo Lisiloshiba ina hadithi kumi na tatu (13) na wahusika ni wafuatao.

TUMBO LISILOSHIBA-Said A. Mohamed

1.     Mzee Mago-Mhusika mkuu
2.     Mwene
3.     Kabwe
4.     Bi. Suruta
5.     Bi. Fambo
6.     Jitu

MAPENZI YA KIFAURONGO-Kenna Wasike
1.     Dennis- Mhusika mkuu
2.     Daktari Mabonga
3.     Penina (mpenzi wa Dennis)
4.     Shakila
5.     Wanafunzi chuoni
6.     Bwana Kitime- babake Penina

SHOGAKE DADA ANA NDEVU-Alifa Chokocho
1.     Safia -mhusika mkuu
2.     Bwana Masudi- babake Safia
3.     Bi. Hamida-mamake Safia
4.     Mkadi (Mtoto wa Habiba Chechei)
5.     Lulua (mnuna wake Safia)
6.     Kimwana (Shogake Safia)

SHIBE INATUMALIZA- Salma Omar Hamad
1.     Sasa
2.     Mbura –wahusika wakuu ni Sasa na Mbura
3.     Mzee Mambo
4.     DJ

MAME BAKARI-Mohammed Khelef Ghassany
1.     Sara –mhusika mkuu
2.     Sarina- rafikiye Sara
3.     Beluwa- dadake Sarina
4.     Bi. Aluwiya- mamake Sara
5.     Babake Sara
6.     Mame Bakari- mtoto aliyezaliwa na Sara
7.     Janadume
8.     Mwalimu Mkuu

Saturday, May 23, 2020

UFAAFU WA ANWANI TUMBO LISILOSHIBA


UFAAFU WA ANWANI TUMBO LISILOSHIBA


Tumbo Lisiloshiba ni anwani ya moja kati ya hadithi zilizotungwa na Said A.  Mohamed. Hadithi hii inapatikana katika kitabu cha hadithi fupi chenye jina Tumbo Lisiloshiba na Hadithi Nyingine. Kitabu hiki kimehaririwa na Alifa Chokocho na Dumu Kayanda.

Kichapishi changu hiki kinaegemea hadithi ya kwanza kwenye kitabu hiki ambayo ni Tumbo Lisiloshiba. Utafiti wangu unachunguza ufaafu wa anwani hii katika hadithi hii. Je, anwani hii inaifaa hadithi hii au la? Bila shaka hoja zifuatazo zinadhibitisha kuwa anwani hii inaiafiki hadithi hii.

Viongozi wamejenga majengo mengi mjini na kumaliza nafasi yote hadi hakuna nafasi ya kuvuta pumzi.

Viongozi wana majengo mengi mjini lakini bado wanahitaji ardhi zaidi ya kujengea majengo mengine.

Kutotosheka kwa matajiri kunawafanya kutaka kuwapokonya Wanamadongoporomoka ardhi zao bila kujali kule ambako maskini hao wangeenda.

Viongozi wameweka vikwazo vya kisheria ili raia wasiweze kuzitetea mali zao baada ya wao kuwanyanganya.

Jitu lina tumbo lisiloshiba kwa vile linaingia mkahawani na kula chakula chote kilichokuwa kimepikwa.

Jitu hilo pia linaagiza kuandaliwa chakula maradufu ambalo lingekuja kula mkahawani siku ambayo ingefuata.

Kwasababu ya kutotosheka kwa viongozi, wanawabomolea raia makazi yao wakiwa wamelala ili waweze kuinyakua ardhi zao.

Tamaa ya viongozi inawafanya kuwatumia askari wa baraza la jiji pamoja na jeshi la polisi ili kuwasaidia kupata ardhi zaidi wakati tayari wana majengo mangi mjini.

Wanasheria wamekosa uaminifu kwa sababu ya tamaa ya pesa. Wanakosa kuwatatulia masikini sharia ngumu zinazowakabili.

Viongozi wanataka kuwalipa Wanamadongoporomoka fidia duni/ visenti vichache ili waondoke Madongoporomoka na kuwaachia ardhi hiyo.

Kutokana na hoja hizi, niko radhi kutoa uamuzi kwamba anwani Tumbo Lisiloshiba inaiafiki hadithi hii. Wawezadondoa hoja zingine ambazo zinadhihirisha kwamba ni kweli anwani hii inaifaa hadithi hii.

GUSA HAPA KUPATA WAHUSIKA KATIKA TUMBO LISILOSHIBA


TOA MAONI AU ULIZA SWALI HAPO KWENYE SEHEMU YA COMMENT 👇

MAUDHUI TAWALA KATIKA TUMBO LISILOSHIBA

Tuesday, May 19, 2020

SAUTI GHUNA NA SIGHUNA

KONSONANTI GHUNA NA SIGHUNA

KONSONANTI GHUNA NA SIGHUNA

Ughuna wa sauti, hasa konsonanti huchunguzwa kwa kuzingatia kigezo cha mtetemeko wa nyuzi sauti.

Mtetemeko wa nyuzi sauti

Kwa kuangalia kigezo cha mtetemeko wa nyuzi sauti, tunapata aina mbili za konsonanti.
      I.          Sauti/ Konsonanti ghuna/nzito
   II.          Sauti/ Konsonanti sighuna/ konsonanti hafifu.

Konsonanti ghuna ni sauti ambazo zinapotamkwa huwa kuna mtatameko/ mtikisiko wa nyuzi sauti.
Mfano wa sauti ghuna ni : /z/, /b/, /g/, /d/, /gh/, /ny/, /ng/, /j/, /v/, /w/, /dh/, /y/, /n/, /m/.

Konsonanti sighuna ni sauti ambazo zinapotamkwa huwa hakuna mtetemeko au mtikisiko wa nyuzi sauti.
 Mfano wa sauti sighuna ni: /s/, /k/, /t/, /p/, /ch/, /f/, /l/, /h/, /th/.


TANBIHI:
Ni muhimu kutambua kwamba sighuna na ghuna hujitokeza katika majozi ya sauti za vitate.
Kwa mfano;
         
          Sighuna       ghuna
          /p/                /b/
          /t/                 /d/
          /th/               /dh/
          /ch/              /j/
          /f/                 /v/
          /k/                /g/
          /kh/              /gh/
          /s/                 /z/
-                       /n/, /ny/, /ng/, /m/
/h/                -
                   /r/, /l/

##MIFANO ZAIDI##

TANBIHI
ü Nazali ghuna ya midomoni-/m/.
ü Nazali ghuna ya ufizi-/n/
ü Nazali ghuna ya kaakaa laini-/ng’/
ü Nazali ghuna ya kaakaa gumu-/ny/
ü Kizuio kwamiza ghuna-/j/
ü Kizuio kwamiza sighuna-/ch/
ü Kipasuo ghuna ya kaakaa laini-/g/
ü Kipasuo sighuna ya kaakaa laini-/k/
ü Kikwamizo ghuna ya midomo na meno-/v/
ü Kikwamizo ghuna  cha ufizi- /z/
ü Kikwamizo sighuna cha midomo na meno-/f/.
ü Kikwamizo sighuna cha ufizi- /s/
ü Kitambaza ghuna cha ufizi-/l/
ü Kikwamizo sighuna cha koromeo-/h/

BONYEZA HAPA KWA FASIHI SIMULIZI

JIKUMBUSHE

VIGEZO VYA KUAINISHA IRABU NI:

  1. Mwinuko wa ulimi (chini, kati, juu)
  2. Mahali pa kutamkia (Mbele, kati au nyuma ya ulimi)
  3. Mkao wa midomo (Mtandazo au mviringo)
VIGEZO VYA KUAINISHA KONSONANTI NI:
  1. Mahali pa kutamkia
  2. Jinsi/ namna ya kutamka
  3. Mtetemeko wa nyuzi sauti
  4. Mkao wa glota/ mkondo hewa

TO SUPPORT US, DONATE TO US ON MPESA 07-02-37-18-29


POST A COMMENT DOWN THERE 👇

Thursday, May 14, 2020

NDOA KATIKA CHOZI LA HERI


MAUDHUI YA NDOA KATIKA CHOZI LA HERI
                            
Ndoa ni makubaliano rasmi ya mwanaume na mwanamke kuishi pamoja kama mume na mke. Pia huitwa chuo. Katika riwaya ya Chozi la Heri, maudhi ya ndoa yanajitokeza baina wahusika mbalimbali. Ndoa hizi zinakumbwa na changamoto tofauti tofuti huku zingine zikisambaratika na zingine zikiimarika. Mifano ya ndoa riwayani ni kama yafuatayo:

Ndoa kati ya Mwimo Msubili na wake zake kumi na wawili akiwemo mamake Ridhaa. Ridhaa ni mmoja wa zao la ndoa hili.

Ndoa kati ya Ridhaa na Terry. Wanaozaliwa kutokana na ndoa hii ni Mwangeka, Annatila(Tila) Dede na Mukeli.

Ndoa kati ya Mwangeka na Lily Nyamvula. Becky anazaliwa kutokana na ndoa hii lakini anaangamia katika mkasa wa kuchomwa kwa jumba la Ridhaa. Lily pia anateketea katika mkasa huo.

Ndoa kati ya Racheal Apondi na Mandu. Wanamzaa Sophie. Mandu anaaga vitani anapoenda kulinda Amani ughaibuni.

Ndoa kati ya Mwangeka na Racheal Apondi baada ya wawili hawa kufiwa na wenzao katika ndoa zao za kwanza. Wanamzaa Ridhaa.

Ndoa kati ya Kaizari na Subira. Lime na Mwanaheri ni mazao ya ndoa  hii.

Ndoa kati ya kangata (mfanyikazi wa Kiriri) na Ndarine. Wanawazaa Lunga Kiriri Kangata, Akelo Kiriri-Kaango na Lucia Kiriri Kangata.

Ndoa kati ya Akelo Kiriri na Kaango. Wawili hawa wanawazaa Ngaire na Mumbi.

Tuesday, May 12, 2020

MABADILIKO SAGAMOYO: KIGOGO

MAUDHUI YA MABADILIKO KATIKA TAMTHILIA YA KIGOGO


Madadiliko mbalimbali yanafanyika katika jumuiya ya Sagamoyo na mengine yanafanywa na wahusika mbalimbali. Baadhi ya mabadiliko ni kama yafuatayo:

Ashua ambaye amekuwa na Sudi katika ndoa ya mapenzi na Amani anabadilika na kusema kuwa Sudi amemchosha na kumwomba talaka. (Uk.47)

Uwanja wa ikulu ya Majoka hujaa pomoni kufikia saa moja asubuhi kila wafanyapo sherehe lakini leo hii siku ya kusherehekea uhuru inayosadifiana na siku ya kuzaliwa kwa Majoka, watu hawajafika uwanjani humu. Ni saa nne lakini kuna watu kumi tu. (Uk.86)

Kingi, mkuu wa polisi ambaye amekuwa akitimiza amri za Majoka leo amebadilika na kukataa kutii Majoka anapomwamuru awapige risasi waliohudhuria mkutano wa Tunu katika lango la soko. Baadaye anajiunga na kikundi wanaouunga mkono Tunu (Uk.90)

Kenga, mshauri mkuu wa Majoka ambaye amekuwa akimsaidia Majoka anamgeuka Majoka na kumwambia kuwa iwapo (Majoka) amekataa kushindwa, basi yeye (Kingi) amekubali. (Uk91)

Mamapima/Asiya aliyepewa kibali cha kuuza pombe haramu kwa kumuunga mkono serikali ya Majoka anabadilika na kumuunga mkono Tunu na kuwaomba Wanasagamoyo msamaha. (Uk.92)

Chopi na Mwango waliokuwa walinzi katika serikali ya Majoka wanamgeuka na kumtoa jukwaani na kumpisha Tunu ili azungumze na Wanasagamoyo. (Uk.92)

Mzee Kenga anabadilika na kumwacha Majoka na kujiunga na umati wa Wanasagamoyo unaomuunga mkono Tunu. (Uk.91)



MAUDHUI TAWALA KATIKA TUMBO LISILOSHIBA
POST A COMMENT DOWN THERE 👇

Monday, May 11, 2020

MBINU REJESHI: CHOZI LA HERI



MBINU REJESHI KATIKA CHOZI LA HERI

Riwaya hii imejengwa kwa kiasi kikubwa kupitia mbinu rejeshi au kisengerenyuma ambayo inajitokeza katika mifano ifuatayo:

1.     Ridhaa anakumbuka kupepesa kwa jicho lake la kulia, anguko aliloanguka sebuleni, mavune yaliyouandama mwili wake na kuunyongonyeza kwa muda, jeshi la kunguru lililotua juu yap aa la maktaba yake, milio ya bundi, kerengende, iliyomtia kiwewe. (Uk.1)

2.     Ridhaa anakumbuka mazungumzo kati yake na Terry mkewe, Terry akimuuliza, “since when has man ever changed his destiny?” (Uk.2)

3.     Ridhaa anakumbuka maneno ya marehemu mamake akimwambia kuwa machozi ya mwanaume hayapaswi kuonekana hata mbele ya majabali ya maisha. (UK.3)

4.     Ridhaa anakumbuka kilio cha mkewe Terry akimwambia Mzee kedi kuwa asiwauwe kwa vile wao ni majirani. (Uk.3)

5.     Ridhaa anakumbuka jinsi mwanawe Mwangeka alivyozaliwa katika chumba chake ambach kwa sasa kimeteketea.(Uk.4)

6.     Ridhaa anakumbuka mjadala kati yake na mwanawe Tila kuhusu mafanikio ya baada ya uhuru. (Uk.5)

7.     Mwandishi kupitia mbinu rejeshi anatueleza jinsi Ridhaa alivyojipata natika Msitu wa Heri, jinsi babake Mzee Mwimo Msubili alivyowahamisha wake zake wawili wa mwisho kutoka Ukungu hadi Ughaishu/Msitu wa Heri. Mamake Ridhaa akiwa ni mmoja wao. (Uk.9)

8.     Ridhaa anakumbuka maneno ya baba yake akimwambia jinsi umiliki wa kibinafsi wa ardhi haukusisitizwa kabla ya miaka hamsini kama ilivyo sasa. (Uk.9)

9.     Ridhaa anakumbuka jinsi wanafunzi wenzake walivyomtenga shuleni na kumuita “mfuata mvua” (Uk. 10)

10.  Ridhaa anakumbuka kuwa Mzee Kedi ndiye aliyemsaidia kupata shamba, kwamba mwanawe Kedi, Mhandisi Kombo ndiye aliyesimamia ujenzi wa nyumba yake, kuwa dadake Kedi ndiye aliyemuuzia shamba na jinsi Terry na mkewe Kedi walivyokuwa kama ndugu wa toka nitoke. (Uk11)

Sunday, May 10, 2020

IMPORTANT YEARS IN THE HISTORY OF THE WORLD

IMPORTANT YEARS IN HISTORY AND GOVERNMENT


 The following are the most important years in history of the world:
1.     1750 
This year marked the beginning of Agrarian revolution. 
Agrarian revolution refers to rapid changes and improvements in the field of agriculture.
Between 1750 and 1850 European countries underwent changes in agriculture.
The changes were marked by:
       i.          A new system of land ownership
     ii.          Use of machines and new farming methods.
The revolution took place first in Britain.
2.     1750-1850
This period marked the Industrial Revolution.
This was a period from 1750 to 1850 where changes in agriculture, manufacturing, mining, transportation, and technology greatly affected the social, economic and cultural conditions of the times.
It began in the United Kingdom, and then subsequently spread throughout Western Europe, Northern America, Japan, and eventually the rest of the world.
In Kenya, it is hoped to be done by 2030.

Characteristics of industrial revolution in Europe

i.          Use of machines to replace human labour.
ii.          The use of steam power to replace water, wind and animal power.
iii.          Increased exploitation and use of coal, iron and steel.
iv.          Rise of the factory system in towns instead of the cottage industries in homes.
v.          Better forms of transport e.g. railways, roads and water.
vi.          Improved living standards and an increase in the human population who required more manufactured goods.
vii.          The production of goods on large scale.
viii.          The development of science and the application of scientific knowledge in production.
ix.          There was development of trade as manufactured goods were sold locally and abroad.
x.          The rise of modern capitalism that provided enough wealth which was then invested back into industry.

3.     1870-1871
This period marked the Franco-Prussian war.
The war was between France and Germany which upset the balance of power in Europe.
 It later led to the outbreak of First World War.

4.     1884-1885