BLOG VISITORS

Showing posts with label Habwe. Show all posts
Showing posts with label Habwe. Show all posts

Saturday, October 23, 2021

UFAAFU WA ANWANI CHECHE ZA MOTO na KAKA BOLLO

 UFAAFU WA ANWANI CHECHE ZA MOTO-MWONGOZO WA CHECHE ZA MOTO

Maana ya cheche-Cheche ni vijisehemu vya kitu chenye mwangaza, vinavyotoa mwanga au mwangaza. Maana ya cheche za moto- Vijisehemu vya moto vinvyoweza kusababisha moto vikiruka na kutua katika mazingira yanayowezakusababisha/ kukuza moto. Katika riwaya ya Cheche za Moto, anwani hii inarejelea vitendo vinavyohatarisha maisha ya wananchi wa kawaida, kuwaletea maumivu au hata vifo. Cheche za moto katika riwaya hii zinatolewa na kiongozi Osman Jumbe, Askari Jeshi, Polisi, kachero wa Osman Jumbe na vyombo vingine vya Dola.

Anwani hii inaifaa riwaya hii kwa sababu inadokeza kwa undani mifano kadhaa ya cheche za moto kama ifuatavyo:

1.   Askari wanampiga Benta risasi kwake nyumbani na kutoweka na mumewe uk 14.

2.   Askari wanambaka mkewe Mule na wengine jumajiana na Mule kishoga uk. 5, 6

3.   Mafuvu ya vichwa vinajazwa kule The Red Valley wakati wa utawala wa Osman Jumbe uk. 5

4.   Askari anamfyatua Mwanakombo risari na kumuua uk. 6/uk. 9

5.   Askari wanawa piga Mule, mkewe na Rita wanapowavamia uk. 3, 5

6.   Wasichana na wavulana wadogo kupigwa risasi uk. 23

7.   Vita kati ya askari Ali na askari jeshi watatu uk. 20

8.   Polisi anamuua kijana kwa kugombania mwanamke vilabuni uk. 25

9.   Osman Jumbe anawaambia Wahindi wa Malanga waondoke warudi kwao uk. 27

10. Masaba anatolewa kwake na askari baaba ya kuambiwa aiage familia yake uk. 35/37    

          KUNA MIFANO MINGINE ZAIDI YA HAMSINI KATIKA MWONGOZO WETU

MWONGOZO HUU PIA UMESHEHENI YAFUATAYO:

1. Wahusika na sifa zao

2. Dhamira ya mwandishi

3. Maudhui na maelezo yao

4. Mbinu za uandishi na mifano yao

5. Maswali ya kudurusu

JIPATIE NAKALA YA MWONGOZO WA CHECHE ZA MOTO 

            NUNUA MWONGOZO WA RIWAYA YA CHECHE ZA MOTO KUTOKA KWETU KWA SHILINGI 500 PEKEE

            BONYEZA HAPA ILI KUNUNUA MWONGOZO-TUMA SHILINGI MIA TANO

PIA TUNAWAPA MAELEKEZO WANAFUNZI KATIKA RIWAYA YA CHECHE ZA MOTO

WASILIANA NASI KWA NAMBARI 0702371829 KWA MAELEZO ZAIDI

ULIZA SWALI AU TOA MAONI KATIKA SEHEMU YA MAONI HAPA CHINIπŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡


Tuesday, June 8, 2021

VITABU VIPYA VYA FASIHI ANDISHI VYA SHULE ZA UPILI 2021

 

VITABU VIPYA VYA FASIHI ANDISHI VYA SHULE ZA UPILI 2021

Subscribe to our Youtube Channel for updates on CHECHE ZA MOTO analysis videos and other updates
Click here> YouTube
Wizara ya Elimu imeidhinisha vitabu vipya vya fasihi andishi vitakavyosomwa, kuchambuliwa na kutahiniwa katika shule za upili kote nchini.

CHECHE ZA MOTO iliyoandikwa na John Habwe na kuchapishwa na Jomo Kenyatta Foundation (JKF) ndiyo riwaya ambayo itachukua nafasi ya riwaya ya Chozi la Heri ya Asumpta K. Matei.

Hadithi fupi, MAPAMBAZUKO YA MACHWEO iliyochapishwa na kampuni ya ushapishaji ya Mountain Top ndiyo itachukua nafasi ya Tumbo Lisiloshiba na hadithi nyingine iliyohaririwa na Alifa Chokocho na Dumu Kayanda.

Wizara ya elimu imeidhinisha vitabu hivi baada ya miaka minne ya kutahiniwa kwa Chozi la Heri na Tumbo Lisiloshiba. 

Wakufunzi wameelezea matarajio makuu kwamba Cheche za Moto huenda ikawa nyepesi kwa wanafunzi kuelewa hasa kwa kuzingatia mtitiriko wa vitushi na idadi ya wahusika. Baadhi ya walimu wamedokeza kwamba riwaya inayoondoka imekuwa changamoto kwao na kwa wanafunzi kwa sababu imeshishirikisha wahusika chungu nzima. Vilevile, walimu hao wameeleza kwamba riwaya Chozi la Heri imekuwa na uchangamano mwingi katika muundo wake.

Kwa upande mwingine, wanafunzi waliohojiwa na Homeschool Kenya wamepongeza watunzi mbalimbali wa hadithi katika diwani ya Tumbo Lisiloshiba. Wanafunzi hao wamedokeza kwamba hadithi hizo mbali na kuburudisha, zimesheheni ujumbe muhimu kwa wanafunzi wote. Nilipowauliza kuhusu changamoto walizokumbana nazo katika usomaji wao wa Tumbo Lisiloshiba, wanafunzi hao walisisitiza kwamba hadithi hizo zimekuwa nyepesi kuelewa.

Tunashughulikia uchambuzi wa Cheche za Moto na Mapambazuko ya Machweo na baada ya siku chache tutachapisha makala hayo humu kwenye blogu kwa manufaa yetu sote. Ahsanteni.

πŸ’«
Wasiliana nasi Kupitia WhatsApp. 

Kwa makala mengine gusa yafuatayo:

NEW BOOK: HOW TO GET AND TEACH FOREIGN STUDENTS ONLINE

 NEW BOOK: HOW TO FIND AND TEACH FOREIGN STUDENTS ONLINE Greetings Mwalimu, and welcome to this educational platform, which has been helping...