BLOG VISITORS

Showing posts with label sarufi. Show all posts
Showing posts with label sarufi. Show all posts

Sunday, January 28, 2024

BEMBEA YA MAISHA: MASWALI MAKUU YA KUDURUSU ILI KUIELEWA RIWAYA KWA KINA

Bembea ya Maisha, iliyoandikwa na mwandishi hodari, Timothy Arege, ni riwaya iliyosheheni maudhui mengi, mbinu nyingi za uandishi, wahusika wengi na mtiririko mzuri wa vitushi. Maswahi haya yatakusaidia kuyaelewa mambo haya kwa undani.


ILI KUPATA MASWALI MENGINE MENGI....BONYEZA HAPA

Thursday, July 16, 2020

SARUFI KIKORONA


MATUMIZI YA LUGHA (Alama 40)
(a) Linanisha na utofautishe sauti zifuatazo           (al.2)
     (i) /th/,/dh/

(c) Tunga sentensi inayodhihirisha           (al.4)
  (i) Nomino ya wingi
  (ii) Kitenzi kishirikishi kuipungufu

(d) Tumia jozi ya maneno yafuatayo kutunga sentenzi moja    (al.2)
  Fumba na vumba

(e) Tofautisha matumizi ya ngali katika sentenzi zifuatazo; (al.2)
      (i) Wanafunzi wangali wanasherehekea
  (ii) Wanafunzi wetu wangalisoma wangalipita mtihani

(f) Tumia ‘O’ rejeshi ili kudhihirisha hali ya mazoea      (al.2)
  Mgonjwa ambaye anakula lishe bora ndiye ambaye atapona haraka

(g) Bainisha aina za virai katika sentensi ifuatayo        (al.3)
   Walimshangilia mgeni wao kwa shangwe

(h) Ainsha viambishi katika neno lifuatalo         (al.3)
   Tutakayempiga

(i) Bianisha aina za yambwa katika sentensi ifuatayo               (al.3)
    Mkulima aliyekata nyasi kwa mundu amewalisha punda

(k) Andika katika usemi halisi                     (al.2)
  Robi alisema kuwa ilikuwa lazima wao waonyeshe heshima kwa watu wote ikiwa walitaka    kuendelea vyema maishani.

(i) Sahihisha sentensi zifuatazo                   (al.2)
   (i) Mbona haujaenda sokoni
(ii) Penye niliandika ni hapo

(m) Andika katika ukubwa              (al.2)
  Wazee hawa wana wake na watoto wengi

(n) Changanua sentensi ifuatayo kwa njia ya visanduku         (al.3)
   Motto aliyekamatwa jana ni mwizi

(o) Unda nomino mbili kutokana na kitenzi ‘chuma’   (al.2)

(p) Andika kinyume cha: (al.2)
  Furaha anajenga nyumba mjini                                                                                                   
(q) Nyambua vitenzi vifuatavyo katika kauli ya kutendeshea na kutendeshwa                            (al.2)
    (i) Fa
   (ii) Nywa

(r) Kanusha sentensi ifuatayo                      (al.1)
  Ningelikuwa na pesa ningelinunua kitanu kile

   ISIMU JAMII (Alama 10)

     Eleza kwa kutolea mifano dhana zofuatazo
     (a) Sajili

     (b) Lafudhi

     (c) Lahaja

     (d) Lingua franka

     (e) Krioli







Tuesday, June 16, 2020

MIUNDO YA NOMINO KATIKA NGELI ZA KISWAHILI


MIUNDO YA NOMINO KATIKA NGELI ZA KISWAHILI
Maana ya ngeli
Ngeli ni makundi mbalimbali ambapo maneno ya Kiswahili yamegwaika. Ni migawo mbalimbali ya maneno ya Kiswahili.

Tanbihi: Katika othografia/ maandishi, ngeli huandikwa kwa herufi kubwa.
Makala haya yanashughulikia miundo mbalimbali ya maneno katika baadhi ya ngeli za Kiswahili.

Ni wazi kwamba maneno tofautitofauti katika ngeli mahususi huchukua maumbo mbalimbali tofauti. Makala haya yanashughulikia maumbo hayo tofauti ya maneno katika ngeli.



NGELI YA A-WA

1.     Muundo wa M-WA- maneno haya huanza kwa M katika umoja na WA katika wingi. Mfano,
mtoto
watoto
mjomba
Wajomba
mwana
Wana
mzee
Wazee
mtemi
watemi

2.     Muundo wa CH-VY. Maneno haya huanza na CH katika umoja VY katika wingi. Mfano,

chura
Vyura



3.     Muundo wa M-MI.

NGELI YA LI-YA

KWA NGELI ZINGINEZO, BONYEZA HAPA

NGELI ZILIZISHUGHULIKIWA:

A-WA
LI-YA
U-ZI
KI-VI
U-I
I-I









Uliza swali moja kwa moja kupitia <WHATSAPP>



Sunday, May 31, 2020

'O' NA 'AMBA' REJESHI: MASWALI NA MAJIBU


 “O” NA “AMBA” REJESHI: MASWALI NA MAJIBU


MAKUENI
Iandike sentensi ifuatayo kwa kutumia ‘O’ rejeshi. (alama 2 )
Kijana ambaye hutumbuiza watu ametuzwa.
JIBU: Kijana atambuizaye watu ametuzwa.

HOMABAY

Unganisha sentensi hizi kwa kutumia kirejeshi cha kati. (alama 2)
(i) Kalamu imeibwa
(ii) Kalamu ni yangu
JIBU: Kalamu iliyoibwa ni yangu

RABAI

Andika sentensi hii upya ukitumia ‘o’ rejeshi tamati.
Zimwi ambalo humla mtu ni lile ambalo linaogopewa. (alama 2)
JIBU: Zimwi lilalo mtu ni lile liogopewalo

KIHARU

Tumia kirejeshi “O” tamati katika sentensi ifuatayo. (alama 1)
Kijana ambaye anapendendeza ni yule ambaye hutia bidii.
JIBU: Kijana apendezaye ni yule atiaye bidii.

NANDI YA KATI

Tunga sentensi ukitumia kirejeshi tamati. (alama 1)
JIBU: Asomaye kwa bidii hufaulu. (alama 1)
(sentensi ionyeshe kuwa kirejeshi tamati huonyesha mazoea)

NANDI KASKAZINI

Tumia ‘amba’ rejeshi katika sentensi ifuatayo: (alama 2)
Mchezaji ninayempenda ni Messi.
JIBU: Mchezaji ambaye ninampenda ni Messi.

NANDI KUSINI –TINDIRET

Kanusha bila kutumia ‘amba’ (alama 2)
Nitamtuza mwanafunzi ambaye ni nadhifu.
JIBU:Sitamtuza mwanafunzi asiye nadhifu.

ELDORET MAGHARIBI

Andika upya bila ya kutumia ‘amba’: (alama 1)
Mtoto ambaye alianguka shimoni ametibiwa.
JIBU: Mtoto aliyeanguka shimoni ametibiwa.

KERICHO

Tumia kirejeshi ‘O’ tamati katika sentesi ifuatayo : (al.2)
Kalamu ambayo alinunua ni ile ambayo anaipenda.
JIBU: Kalamu ainunuayo ni ile aipendayo

NANDI KATI

Tumia ‘amba’ katika sentensi ifuatayo. (alama 1)
Wanafunzi wapitao mtihani husherehekea.
JIBU: Wanafunzi ambao hupita mtihani husherehekea.

KEIYO

Sunday, May 24, 2020

WAHUSIKA KATIKA TUMBO LISILOSHIBA

WAHUSIKA KATIKA TUMBO LISILOSHIBA


Katika fasihi, mhusika ni kiumbe aliyefasiriwa au kubuniwa na mtunzi, anayemwiga na kufanana na kiumbe halisi duniani kwa kiasi Fulani. Kuna aina mbalimbali za wahusika kama vile:

a)    Mhusika mkuu

Huyu ni mhusika ambaye anajitokeza katika hadithi kwa kiasi kikubwa zaidi kuliko wahusika wengine. Huweza kujitokeza kuanzia mwanzo hadi mwisho wa hadithi.

b)    Wahusika wadogo/ wasaidizi

Hawa ni wahusika ambao hutangamana na mhusika mkuu na kumsaidia kuibua dhamira na maudhui katika hadithi. Wahusika hawa hujitokeza kwa kiasi kidogo tu kwenya hadithi na kisha kupotea.

Diwani ya Tumbo Lisiloshiba ina hadithi kumi na tatu (13) na wahusika ni wafuatao.

TUMBO LISILOSHIBA-Said A. Mohamed

1.     Mzee Mago-Mhusika mkuu
2.     Mwene
3.     Kabwe
4.     Bi. Suruta
5.     Bi. Fambo
6.     Jitu

MAPENZI YA KIFAURONGO-Kenna Wasike
1.     Dennis- Mhusika mkuu
2.     Daktari Mabonga
3.     Penina (mpenzi wa Dennis)
4.     Shakila
5.     Wanafunzi chuoni
6.     Bwana Kitime- babake Penina

SHOGAKE DADA ANA NDEVU-Alifa Chokocho
1.     Safia -mhusika mkuu
2.     Bwana Masudi- babake Safia
3.     Bi. Hamida-mamake Safia
4.     Mkadi (Mtoto wa Habiba Chechei)
5.     Lulua (mnuna wake Safia)
6.     Kimwana (Shogake Safia)

SHIBE INATUMALIZA- Salma Omar Hamad
1.     Sasa
2.     Mbura –wahusika wakuu ni Sasa na Mbura
3.     Mzee Mambo
4.     DJ

MAME BAKARI-Mohammed Khelef Ghassany
1.     Sara –mhusika mkuu
2.     Sarina- rafikiye Sara
3.     Beluwa- dadake Sarina
4.     Bi. Aluwiya- mamake Sara
5.     Babake Sara
6.     Mame Bakari- mtoto aliyezaliwa na Sara
7.     Janadume
8.     Mwalimu Mkuu

Tuesday, May 19, 2020

SAUTI GHUNA NA SIGHUNA

KONSONANTI GHUNA NA SIGHUNA

KONSONANTI GHUNA NA SIGHUNA

Ughuna wa sauti, hasa konsonanti huchunguzwa kwa kuzingatia kigezo cha mtetemeko wa nyuzi sauti.

Mtetemeko wa nyuzi sauti

Kwa kuangalia kigezo cha mtetemeko wa nyuzi sauti, tunapata aina mbili za konsonanti.
      I.          Sauti/ Konsonanti ghuna/nzito
   II.          Sauti/ Konsonanti sighuna/ konsonanti hafifu.

Konsonanti ghuna ni sauti ambazo zinapotamkwa huwa kuna mtatameko/ mtikisiko wa nyuzi sauti.
Mfano wa sauti ghuna ni : /z/, /b/, /g/, /d/, /gh/, /ny/, /ng/, /j/, /v/, /w/, /dh/, /y/, /n/, /m/.

Konsonanti sighuna ni sauti ambazo zinapotamkwa huwa hakuna mtetemeko au mtikisiko wa nyuzi sauti.
 Mfano wa sauti sighuna ni: /s/, /k/, /t/, /p/, /ch/, /f/, /l/, /h/, /th/.


TANBIHI:
Ni muhimu kutambua kwamba sighuna na ghuna hujitokeza katika majozi ya sauti za vitate.
Kwa mfano;
         
          Sighuna       ghuna
          /p/                /b/
          /t/                 /d/
          /th/               /dh/
          /ch/              /j/
          /f/                 /v/
          /k/                /g/
          /kh/              /gh/
          /s/                 /z/
-                       /n/, /ny/, /ng/, /m/
/h/                -
                   /r/, /l/

##MIFANO ZAIDI##

TANBIHI
ü Nazali ghuna ya midomoni-/m/.
ü Nazali ghuna ya ufizi-/n/
ü Nazali ghuna ya kaakaa laini-/ng’/
ü Nazali ghuna ya kaakaa gumu-/ny/
ü Kizuio kwamiza ghuna-/j/
ü Kizuio kwamiza sighuna-/ch/
ü Kipasuo ghuna ya kaakaa laini-/g/
ü Kipasuo sighuna ya kaakaa laini-/k/
ü Kikwamizo ghuna ya midomo na meno-/v/
ü Kikwamizo ghuna  cha ufizi- /z/
ü Kikwamizo sighuna cha midomo na meno-/f/.
ü Kikwamizo sighuna cha ufizi- /s/
ü Kitambaza ghuna cha ufizi-/l/
ü Kikwamizo sighuna cha koromeo-/h/

BONYEZA HAPA KWA FASIHI SIMULIZI

JIKUMBUSHE

VIGEZO VYA KUAINISHA IRABU NI:

  1. Mwinuko wa ulimi (chini, kati, juu)
  2. Mahali pa kutamkia (Mbele, kati au nyuma ya ulimi)
  3. Mkao wa midomo (Mtandazo au mviringo)
VIGEZO VYA KUAINISHA KONSONANTI NI:
  1. Mahali pa kutamkia
  2. Jinsi/ namna ya kutamka
  3. Mtetemeko wa nyuzi sauti
  4. Mkao wa glota/ mkondo hewa

TO SUPPORT US, DONATE TO US ON MPESA 07-02-37-18-29


POST A COMMENT DOWN THERE 👇

SPECIAL FEATURE-PHOTOSYNTHESIS

  PHOTOSYNTHESIS AND WHY IT IS IMPORTANT Photosynthesis and Why it is Necessary Photosynthesis is a critical process that sustains plants ...