BLOG VISITORS

Showing posts with label arudhi. Show all posts
Showing posts with label arudhi. Show all posts

Saturday, August 16, 2025

NEW BOOK: HOW TO GET AND TEACH FOREIGN STUDENTS ONLINE

 NEW BOOK: HOW TO FIND AND TEACH FOREIGN STUDENTS ONLINE


Greetings Mwalimu, and welcome to this educational platform, which has been helping students and teachers since 2020.

My name is Victor Bollo, a seasoned teacher of Kiswahili and History with over five years of experience.

Today, I present to you this life-changing book, Getting and Teaching Foreign Students Online, in response to endless requests from many teachers who are ardent readers and beneficiaries of this platform.

If you are interested or passionate about teaching foreign students online, on part time or full-time basis to earn extra income, this book is for you.

The book goes for only Kshs. 250.

It has 8 chapters and below is its outline:

  1. Chapter 1: Introduction: The Rising Global Demand for Online Learning and Why African Teachers Are Well-Positioned for Online Teaching
  2. Chapter 2: Most In-Demand Subjects for Foreign Students (With Percentage Demand)
  3. Chapter 3: Where to Find Foreign Students Online (We have provided working URL Links to sites that have worked for us)
  4. Chapter 4: Essential Requirements for Successful Online Teaching (What else apart from your smart phone or laptop)
  5. Chapter 5: Steps to Start Teaching & Growing Your Student Base
  6. Chapter 6: Common Mistakes & How to Avoid Them
  7. Chapter 7: Advanced Strategies for Scaling & Long-Term Success
  8. Chapter 8: Conclusion & Final Tips for Long-Term Success

Final Words: Your Journey Starts Now

This book has been authored by a small team of experienced teachers, including those who are currently teaching in international schools such as Nova Pioneer Academy, The Agakhan Academy, and Brookhurst International School Academy. 

The teachers have created working connections with international students and have indicated strategies that have helped them get and teach foreign students.

The entire book is Kshs. 250

A chapter is Kshs. 100

Click below to buy and receive a PDF copy directly on your Whatsapp.

πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡

BUY THE WHOLE BOOK


BUY A CHAPTER 
OF THE BOOK


For comprehensive notes and other materials click πŸ‘‰HERE

Any question or comment, please post it down here πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡




Tuesday, July 22, 2025

SHAMIRISHO KATIKA KISWAHILI (KIPOZI, KITONNDO, NA ALA)

 

SHAMIRISHO KATIKA KISWAHILI

SHAMIRISHO KATIKA KISWAHILI

MAANA YA SHAMIRISHO:

Shamirisho ni neno ambalo huashiria nomino inayopokea kitendo (kitendwa/mtendwa), nonimo inayofaidika kutokana na kitendo (kitendewa/mtendewa), na kifaa kinachotumika katika kitendo (ala), katika sentensi.

AINA ZA SHAMIRISHO

1. Shamirisho Kipozi/ Yambwa Tendwa

2. Shamirisho Kitondo/ Yambwa Tendewa/yambiwa

3. Shamirisho Ala/ Kitumizi

------------------------------------------------------------------------------

1. SHAMIRISHO KIPOZI

Pia huitwa yambwa tendwa (Direct object).
Ni nomino anayopokea athari ya kitendo moja kwa moja.
Mara nyingi hipatikana katika sentensi zilizoandikwa katika kauli ya kutenda, japo huwezakupatikana katika sentensi zilizoandikwa katika kauli zingine.

Mifano

  1. Wizara ya elimu inarekebisha mtaala. (mtaala-shamirisho kipozi)
  2. Mkulima analima shamba.  (shamba-shamirisho kipozi)
  3. Mgonjwa aliletewa chai kwa chupa na Swaleh. 
  4. Kitabu cha mwanafunzi kimepotezwa na mtoto.
  5. Kipenga cha mkufunzi kitanunuliwa wiki ijayo na mwalimu mkuu.
----------------------------------------------------------------------
----------------------------------------------------------------------
2. SHAMIRISHO KITONDO
Pia huitwa yambwa tendewa au yambiwa (Indirect Object).
Ni nomino ambayo huathiriwa na kitendo kwa njia isiyo ya moja kwa moja.
Huathiriwa na kitendo kinacho tendwa kwa shamirisho kipozi.
Hupatikana katika sentensi zilizoandikwa katika kauli ya kitendea/ kutendewa.

Mifano
  1. Mzazi alimnunulia mwanawe baiskeli kwa kupita mtihani.
  2. Kaka atamfyekea babu yangu shamba baada ya kutoa mahindi.
  3. Nina alimpikia mgonjwa chakula chenye ladha tamu.
  4. Walimu waliwekewa runinga kwanye afisi yao.
  5. Mwanasiasa alipigiwa kura na kushinda uchaguzi mdogo wa mkoa.
----------------------------------------------------------------------
3. SHAMIRISHO ALA/ KITUMIZI
Ni nomino ambayo hurejelea kifaa kinachotumiwa kitekeleza kitendo fulani.
Huwakilishwa na vielezi vya namna ala.
KUMBUKA: "kwa" si sehemu ya shamirisho ala.

Mifano
  1. Kaka alilima shamba lake kwa jembe jipya.
  2. Mpishi alikata vitunguu na nyanya kwa kisu.
  3. Mwalimu alisahihisha vitabu vya wanafunzi kwa kalamu.
  4. Juma alisafiri ughaibuni kwa ndege.
  5. Viwanja vilinunuliwa kwa pesa
  6. Mkongwe atajengewa nyumba ya mbao.
----------------------------------------------------------------------
----------------------------------------------------------------------
SHUKRAN KWA USOMAJI WAKO πŸ™πŸ‘πŸ˜Ž

UNA SWALI KUHUSU SHAMIRISHO KIPOZI, KITONDO, AMA SHAMIRISHO ALA?
ULIZA HAPA CHINI πŸ‘‡πŸ‘‡


Tuesday, June 8, 2021

VITABU VIPYA VYA FASIHI ANDISHI VYA SHULE ZA UPILI 2021

 

VITABU VIPYA VYA FASIHI ANDISHI VYA SHULE ZA UPILI 2021

Subscribe to our Youtube Channel for updates on CHECHE ZA MOTO analysis videos and other updates
Click here> YouTube
Wizara ya Elimu imeidhinisha vitabu vipya vya fasihi andishi vitakavyosomwa, kuchambuliwa na kutahiniwa katika shule za upili kote nchini.

CHECHE ZA MOTO iliyoandikwa na John Habwe na kuchapishwa na Jomo Kenyatta Foundation (JKF) ndiyo riwaya ambayo itachukua nafasi ya riwaya ya Chozi la Heri ya Asumpta K. Matei.

Hadithi fupi, MAPAMBAZUKO YA MACHWEO iliyochapishwa na kampuni ya ushapishaji ya Mountain Top ndiyo itachukua nafasi ya Tumbo Lisiloshiba na hadithi nyingine iliyohaririwa na Alifa Chokocho na Dumu Kayanda.

Wizara ya elimu imeidhinisha vitabu hivi baada ya miaka minne ya kutahiniwa kwa Chozi la Heri na Tumbo Lisiloshiba. 

Wakufunzi wameelezea matarajio makuu kwamba Cheche za Moto huenda ikawa nyepesi kwa wanafunzi kuelewa hasa kwa kuzingatia mtitiriko wa vitushi na idadi ya wahusika. Baadhi ya walimu wamedokeza kwamba riwaya inayoondoka imekuwa changamoto kwao na kwa wanafunzi kwa sababu imeshishirikisha wahusika chungu nzima. Vilevile, walimu hao wameeleza kwamba riwaya Chozi la Heri imekuwa na uchangamano mwingi katika muundo wake.

Kwa upande mwingine, wanafunzi waliohojiwa na Homeschool Kenya wamepongeza watunzi mbalimbali wa hadithi katika diwani ya Tumbo Lisiloshiba. Wanafunzi hao wamedokeza kwamba hadithi hizo mbali na kuburudisha, zimesheheni ujumbe muhimu kwa wanafunzi wote. Nilipowauliza kuhusu changamoto walizokumbana nazo katika usomaji wao wa Tumbo Lisiloshiba, wanafunzi hao walisisitiza kwamba hadithi hizo zimekuwa nyepesi kuelewa.

Tunashughulikia uchambuzi wa Cheche za Moto na Mapambazuko ya Machweo na baada ya siku chache tutachapisha makala hayo humu kwenye blogu kwa manufaa yetu sote. Ahsanteni.

πŸ’«
Wasiliana nasi Kupitia WhatsApp. 

Kwa makala mengine gusa yafuatayo:

Tuesday, April 14, 2020

USHAIRI: SHAIRI HURU


MFANO WA SHAIRI HURU


SEHEMU YA A: USHAHIRI
                                    SHAIRI ‘A’
            (i)                    Umekata mti mtima
                                    Umeangukia nyumba yako
                                    Umeziba mto hasira
                                    Nyumba yako sasa mafurikoni
                                    Na utahama
                                    Watoto wakukimbilia

            (ii)                   Mbuzi kumkaribia chui
                                    Alijigeuza panya
                                    Akalia kulikuwa na paka
                                    Kichwani
                                    Mchawi kutaka sama kutisha
                                    Alijigeuza samba
                                    Akalia na risasi kichwani

            (iii)                  Jongoo wapi sasa yatakwenda
                                    Bwanako kumpa sumu?
                                    Hadija umeshika nyoka kwa mkia
                                    Hadija umepitia nyuma ya punda
Jogoo kataka sana kukimbia
Aliomba miguu elfu

(iv)                  Akaachwa na nyoka
Hadija wapi sasa
Bwanako kumpa sumu?
Hadija umashika nyoka kwa mkia
Hadija amepita nyuma ya punda

SHAIRI ‘B’
                                    Piteni jamani,piteni haraka
                                    Nendeni ,nendeni huko mwendako
                                    Mimi haraka, haraka sina
                                    Mzigo wangu,mzigo mzito mno
                                    Na chui sitaki kuweka

                                    Vijana kwa nini hampiti?
                                    Kwa nini mwanicheka kisogo?
                                    Mzigo niliobeba haupo.

                                    Lakini umenipinda mgongo na
                                    Nendako
                                    Haya piteni!piteni haraka!Heei!

                                    Mwafikiri mwaniacha nyuma!
                                    Njia ya maisha ni moja tu.
                                    Huko mwendako ndiko nilikotoka
                                    Na nilipofikia wengi wenu
                                    Hawatafika

                                    Kula nimekula na sasa mwasema
                                    Niko nyuma ya wakati
                                    Lakini kama mungepita mbele
                                    Na uso wangu kutazama
                                    Ningemwambia siri ya miaka
                                    Mingi

Maswali
(a)Haya ni mashairi ya aina gani?Toa sababu.     (Alama 2)

(b)Washairi hawa wawili wanalalamika.Yafafanue malalamishi yao.             (Alama 4)

(c)Onyesha jinsi kinaya kinavyotokeza katika tungo hizi mbili. (Alama4)                                                                                                                                         
(d)       Ni vipi Hadija :-
  (i) Amekata mti mtima?    (Alama 2)                                              
 (ii)       Amepita nyuma ya punda. (Alama 2)

(e) Toa mifano miwili ya uhuru mshairi kwa kurejelea mashairi haya.            (Alama 2)

(f)        kwa kurejelea shairi ‘B’ eleza maana ya:-
                                    (i)        Mzigo
                                    (ii)       Siri
                                    (iii)      Kula nimekula
           (iv)      Niko nyuma ya wakati.(Alama 4)
                                           
###KWA MASWALI YA FASIHI SIMULIZI, GUSA HAPA###

###KWA MASWALI YA KIGOGO, BONYEZA HAPA###

###KWA MASWALI YA TUMBO LISILOSHIBA, GUSA HAPA###

Uliza swali moja kwa moja kupitia <WHATSAPP>

POST A COMMENT DOWN THERE πŸ‘‡

NEW BOOK: HOW TO GET AND TEACH FOREIGN STUDENTS ONLINE

 NEW BOOK: HOW TO FIND AND TEACH FOREIGN STUDENTS ONLINE Greetings Mwalimu, and welcome to this educational platform, which has been helping...