BLOG VISITORS

Friday, May 1, 2020

UTAFITI NYANJANI: UKUSANYAJI WA DATA YA FASIHI SIMULIZI


UTAFITI NYANJANI: UKUSANYAJI WA DATA YA FASIHI SIMULIZI
Hiki ni kitendo cha kwenda katika jamii fulani na kukusanya data inayohitajika na kuichambua.

UMUHIMU WA UTAFITI NYANJANI KATIKA FASIHI SIMULIZI
ü  Huwezesha kuendelezwa kwa utamaduni wa jamii mbalimbali
ü  Hukuza na kuendeleza somo la fasihi simulizi.
ü  Huzia kupotea kwa fasihi simulizi.
ü  Hushughulikia mambo mapya ambayo hayakushughulikiwa hapo mwanzoni.
ü  Hukuza na kusambaza maarifa na ujumbe wa fasihi simulizi kwa jamii pana.
ü  Humpa mwanafunzi mbinu za utafiti anazoweza kutumia katika masomo mengine.
ü  Huibua na kukuza vipawa vya watafiti kama vile utambaji, uigizaji, usogora na kadhalika.

HATUA ZA KUFANYA UTAFITI

1)    Maandalizi: Huhusisha mambo yafuatayo:
             i. Uteuzi wa mada ya utafiti
             ii. Kubainisha na kueleza malengo ya utafiti huo.
             iii. Kutambia eneo la kufanyia utafiti
            iv. Kutambua utafiti ambao tayari ulifanywa kuhusu mada yako.
             v. Kukadiria gharama katika shughuli nzima.

2)    Ukusanyaji wa Data yenyewe
Ukusanyaji unawezakufanywa kupitia jia hizi:
ü  Kushuhudia
ü  Kujaza fomu
ü  Kushiriki
ü  Kuhoji nk

3)    Kurekodi Data yako
Unahitaji kurekodi data zako kupitia njia zifuatazo:
ü  Kuandika
ü  Kupiga picha
ü  Kuchukua video
ü  Kunasa habari nk

4)    Kuchunguza Data
Data ambayo umekusanya inahitaji kuchunguzwa, kufsiriwa na kuandikwa upya, neno baada ya neno ili maana halisi inayokusudiwa isipotezwe.

5)    Kuchambua na kufasili Data
Data uliyokusanya inahitaji kuchambuliwa, kulinganishwa, kufasiliwa, kutathminiwa na kisha kujumuishwa ili kupata matokeo kamili ya utafiti wako.

TO SUPPORT US, DONATE TO US ON MPESA 07-02-37-18-29


MBINU ZA KUKUSANYA DATA


1.     KUSHUHUDIA/KUTAZAMA/UCHUNGUZAJI
Katika mbinu hii, mtafiti husimama kando na kurekodi utendaji/ matendo yanayoendelea katika jamii anayotafiti.

2.     KUSHIRIKI
Mtafiti hujihushisha na kuchangia katika utendaji wa shughuli inayofanywa na wanajamii inayotafitiwa.
Mbinu ya kushiriki ni muhimu kwa sababu:
Ø  Hukuza ushirikiano na mlahaka mzuri baina ya mtafiti na watafitiwa.
Ø  Huleta jamii inayotafitiwa karibu na kumfanya mtafiti kuwa huru kuwauliza maswali.
Ø  Humwezesha mtafiti kusisimka/kufurahia shughuli hiyo ya utendaji.

3.     MAHOJIANO/USAILI
Huhushisha mtafiti kumhoji/kumuuliza swali mtafitiwa, ili kupata majibu (data) ya maswala anayoyatafitia.

4.     HOJAJI/FOMU YA MASWALI
Mtafiti huandaa hojaji kabla ya kwenda nyanjani na kuwapa watu kujaza. Pia, mchunguzi anaweza kumhoji mtu na kujaza hojaji mwenyewe.

5.     UTAFITI MAKTABANI
Huhusisha kuchunguza na kupitia mambo ambayo tayari yameandiwa vitabuni, mtandaoni na kwenye majarida kuhusu mada unayotafitia.

               MBINU ZA KUREKODI NA KUHIFADHI DATA
Mbinu hizi zimegawika katika makundi mawili kv:
                           i.          Mbinu za zamani
                         ii.          Mbinu za kisasa
Mbinu za kizamani
a)    Kuhifadhi mongoni/akili

SWALI: Eleza udhaifu/ changamoto za kuhifadhi data akilini.
ü  Mtafiti/ fanani huwezakufa
ü  Mtafiti huwezakusahau maswala aliyoweka akilini
ü  Mtafiti huwezakuathirika kiakili
ü  Mtafiti huweza kubadili aliyohifadhi akilini
ü  Mfatiti/fanani huwezakupoteza fahamu

Mbinu za kisasa
SWALI: Taja mbinu za kisasa za kuhifadhi data.
i.                 Kutumia kanda za kunasa sauti
ii.               Video
iii.             Maandishi
iv.             Filamu
v.               Kupiga picha kutumia kamera
vi.             Tepu-rekoda
vii.           Sidi

SWALI: Eleza matatizo/ changamoto za kutumia mbinu za kisasa kuhifadhi data.
ü  Huhitaji ujuzi wa kutumia vifaa hivi.
ü  Ni ghali/ huwa na gharama ya juu.
ü  Huwezakupoteza data muhimu zikuharibika
ü  Haziwezi kufanya kazi bila nguvu za umeme

MATATIZO AMBAYO HUWAKUMBA WATAFITI WAKIWA NYANJANI KUKUSANYA DATA
SWALI: Eleza matatizo ambayo mtafiti huweza kukumbana nayo akiwa nyanyani.
                   i.          Kutoelewa lugha ya jamii anayotafiti
                 ii.          Vifaa vya kutafitia kuharibika ama kupotea
               iii.          Changamoto za usafiri
                iv.          Jamii husika inaweza kumshuku mtafiti kuwa anawapepeleza na hivyo kubadili tabia.
                  v.          Washiriki huwezakuhitaji kulipwa pesa.
                vi.          Kukosa ruhusa kutoka kwa vyombo vya dola kama vile polisi ambao huwezakuchochea shughuli ya kukusanya data.
              vii.          Hali mbaya ya anga kama vile mvua kunyesha zaidi na kuzuia utafiti kuendelea.


                  HISTORY MARKING SCHEMES


POST A COMMENT DOWN THERE 👇

39 comments:

  1. PONGEZI KWA KAZI NZURI NA KWA UJUMBE MUHIMU KWETU WANAFUNZI TUNATARAJIA MENGI MAZUZI

    ReplyDelete
  2. Kazi nzuri, iwapo kuna yeyote anayeweza kunijuza na Umuhimu wa maandalizi kabla ya utafiti.Nitashukuru sana

    ReplyDelete
  3. Kwa uchambuzi zaidi, majibu ya maswali na makala mengine, subscribe channel yetu ye YoutTube hapa.

    https://www.youtube.com/channel/UC3EEBQNhW-y6VNg3JgpN76Q

    ReplyDelete
  4. nimeelimika sana na makala haya .asante

    ReplyDelete
  5. Hongera kabisa,kazi nzuri hio ,na nawahiza mwendelee kutia bidiii zaidi . Asanteni🙏

    ReplyDelete
  6. Asante sana mwalimu ...imenisaidia katika kazi ya likizo

    ReplyDelete
  7. Good work you are really helpful

    ReplyDelete
  8. Kazi murua zaidi,imenifutia na kufanya kulipenda hili somo,natumai ungekuwa mwalimu wangu enzi zile.

    ReplyDelete
  9. 𝔸𝕤𝕒𝕟𝕥 𝕤𝕒𝕟𝕒

    ReplyDelete
  10. Pongezi kwa kazi nzuri

    ReplyDelete
  11. Kazi kuntu. Kongole!

    ReplyDelete
  12. Asante sana mwalimu......imenisaidia sana katika kazi ya likizo

    ReplyDelete
  13. Thanks for good work

    ReplyDelete
  14. Good work may God bless


    you

    ReplyDelete
  15. Kazi ya kiwango Cha juu Sana,,vyema

    ReplyDelete
  16. Kongole, kazi nzuri

    ReplyDelete

SPECIAL FEATURE-PHOTOSYNTHESIS

  PHOTOSYNTHESIS AND WHY IT IS IMPORTANT Photosynthesis and Why it is Necessary Photosynthesis is a critical process that sustains plants ...