BLOG VISITORS

Sunday, May 31, 2020

'O' NA 'AMBA' REJESHI: MASWALI NA MAJIBU


 “O” NA “AMBA” REJESHI: MASWALI NA MAJIBU


MAKUENI
Iandike sentensi ifuatayo kwa kutumia ‘O’ rejeshi. (alama 2 )
Kijana ambaye hutumbuiza watu ametuzwa.
JIBU: Kijana atambuizaye watu ametuzwa.

HOMABAY

Unganisha sentensi hizi kwa kutumia kirejeshi cha kati. (alama 2)
(i) Kalamu imeibwa
(ii) Kalamu ni yangu
JIBU: Kalamu iliyoibwa ni yangu

RABAI

Andika sentensi hii upya ukitumia ‘o’ rejeshi tamati.
Zimwi ambalo humla mtu ni lile ambalo linaogopewa. (alama 2)
JIBU: Zimwi lilalo mtu ni lile liogopewalo

KIHARU

Tumia kirejeshi “O” tamati katika sentensi ifuatayo. (alama 1)
Kijana ambaye anapendendeza ni yule ambaye hutia bidii.
JIBU: Kijana apendezaye ni yule atiaye bidii.

NANDI YA KATI

Tunga sentensi ukitumia kirejeshi tamati. (alama 1)
JIBU: Asomaye kwa bidii hufaulu. (alama 1)
(sentensi ionyeshe kuwa kirejeshi tamati huonyesha mazoea)

NANDI KASKAZINI

Tumia ‘amba’ rejeshi katika sentensi ifuatayo: (alama 2)
Mchezaji ninayempenda ni Messi.
JIBU: Mchezaji ambaye ninampenda ni Messi.

NANDI KUSINI –TINDIRET

Kanusha bila kutumia ‘amba’ (alama 2)
Nitamtuza mwanafunzi ambaye ni nadhifu.
JIBU:Sitamtuza mwanafunzi asiye nadhifu.

ELDORET MAGHARIBI

Andika upya bila ya kutumia ‘amba’: (alama 1)
Mtoto ambaye alianguka shimoni ametibiwa.
JIBU: Mtoto aliyeanguka shimoni ametibiwa.

KERICHO

Tumia kirejeshi ‘O’ tamati katika sentesi ifuatayo : (al.2)
Kalamu ambayo alinunua ni ile ambayo anaipenda.
JIBU: Kalamu ainunuayo ni ile aipendayo

NANDI KATI

Tumia ‘amba’ katika sentensi ifuatayo. (alama 1)
Wanafunzi wapitao mtihani husherehekea.
JIBU: Wanafunzi ambao hupita mtihani husherehekea.

KEIYO

SPECIAL FEATURE-PHOTOSYNTHESIS

  PHOTOSYNTHESIS AND WHY IT IS IMPORTANT Photosynthesis and Why it is Necessary Photosynthesis is a critical process that sustains plants ...