BLOG VISITORS

Friday, May 1, 2020

UTAFITI NYANJANI: UKUSANYAJI WA DATA YA FASIHI SIMULIZI


UTAFITI NYANJANI: UKUSANYAJI WA DATA YA FASIHI SIMULIZI
Hiki ni kitendo cha kwenda katika jamii fulani na kukusanya data inayohitajika na kuichambua.

UMUHIMU WA UTAFITI NYANJANI KATIKA FASIHI SIMULIZI
ü  Huwezesha kuendelezwa kwa utamaduni wa jamii mbalimbali
ü  Hukuza na kuendeleza somo la fasihi simulizi.
ü  Huzia kupotea kwa fasihi simulizi.
ü  Hushughulikia mambo mapya ambayo hayakushughulikiwa hapo mwanzoni.
ü  Hukuza na kusambaza maarifa na ujumbe wa fasihi simulizi kwa jamii pana.
ü  Humpa mwanafunzi mbinu za utafiti anazoweza kutumia katika masomo mengine.
ü  Huibua na kukuza vipawa vya watafiti kama vile utambaji, uigizaji, usogora na kadhalika.

HATUA ZA KUFANYA UTAFITI

1)    Maandalizi: Huhusisha mambo yafuatayo:
             i. Uteuzi wa mada ya utafiti
             ii. Kubainisha na kueleza malengo ya utafiti huo.
             iii. Kutambia eneo la kufanyia utafiti
            iv. Kutambua utafiti ambao tayari ulifanywa kuhusu mada yako.
             v. Kukadiria gharama katika shughuli nzima.

2)    Ukusanyaji wa Data yenyewe
Ukusanyaji unawezakufanywa kupitia jia hizi:
ü  Kushuhudia
ü  Kujaza fomu
ü  Kushiriki
ü  Kuhoji nk

3)    Kurekodi Data yako
Unahitaji kurekodi data zako kupitia njia zifuatazo:
ü  Kuandika
ü  Kupiga picha
ü  Kuchukua video
ü  Kunasa habari nk

4)    Kuchunguza Data
Data ambayo umekusanya inahitaji kuchunguzwa, kufsiriwa na kuandikwa upya, neno baada ya neno ili maana halisi inayokusudiwa isipotezwe.

5)    Kuchambua na kufasili Data
Data uliyokusanya inahitaji kuchambuliwa, kulinganishwa, kufasiliwa, kutathminiwa na kisha kujumuishwa ili kupata matokeo kamili ya utafiti wako.

TO SUPPORT US, DONATE TO US ON MPESA 07-02-37-18-29


MBINU ZA KUKUSANYA DATA

SPECIAL FEATURE-PHOTOSYNTHESIS

  PHOTOSYNTHESIS AND WHY IT IS IMPORTANT Photosynthesis and Why it is Necessary Photosynthesis is a critical process that sustains plants ...