BLOG VISITORS

Thursday, April 30, 2020

UFAAFU WA ANWANI-CHOZI LA HERI

UFAAFU WA ANWANI-CHOZI LA HERI


Chozi ni matone ya maji yanayotoka kwenye jicho/macho ya mtu kutokana na maumivu au furaha. Heri ni hali ya kuwa salama au hali ya kupata jambo jema. Pia linamaanisha nafuu au afadhali. Maneno haya yakiunganishwa pamoja yanaleta maana ya chozi linalomtoka mtu wakati hali imakuwa salama au kupata jambo zuri. Au chozi analotoa mtu hali inapokuwa nafuu au afadhali kwake.

Hoja zifuatazo zinathibitisha ufaafu wa anwani hii ya Chozi la Heri.

1.     Familia ya mzee Mwimo Msubili inateseka kutokana na udogo wa ardhi lakini hali inakuwa nzuri babake Ridhaa anapowahamisha wake zake wawili wa mwisho, katika Msitu wa Heri. Mmoja wa hawa ni mamake Ridhaa.

2.     Ridhaa anadhulumiwa na wanafunzi wenzake shulenina kutukanwa kuwa yeye ni mfuata mvua lakini hali inakuwa nzuri baada yamamake kwenda na kuzungumza na mwalimu mkuu na hali nii kusitishwa.

3.     Eneo la Msitu wa Heri lilikuwa kame (Kalahari) lakini inageuka kuwa nzuri baada ya Ridhaa kuwaletea maji ya mabomba na eneo hilo kutwaa rangi ya kichani kiwiti.

4.     Hali inakiwa nsuri kwa Mzee Kedi Ridhaa anapoyathamini masomo ya wapwa zake wawili.

5.     Mwekevu anapoingia kwenye siasa anatusiwa na watu lakini hali hii inabadilika na kuwa bora baada ya kushinda uchaguzi.

6.     Familia ya Kaizari inapata taabu anapovamiwa na wahuni lakini anapata heri wakati jirani yake Tulia anapomsaidia kutorokea palipo salama.

7.     Kaizari anapovamiwa na mkewe Subira kujeruhiwa na wananwe Lime na Mwanaheri kubakwa, anapata heri Tulia anapojitolea kumlindia nyumba isije ikaharibiwa na wahuni.

8.     Wakimbizi wanapoteseka kambini kutokana na ukosefu wa chakula, misikiti na makanisa yana waletea chakula na kuwafanya kuona heri.

9.     Wakimbizi wanapoteseka kwa kulala vibandani, shirika la Makazi Bora linajitolea kuwajengea makao bora.

10.  Selume anapotaabika baada ya kukataliwa na mumewe Mwanzi, anakutana na Ridhaa anayemsaidia kupata kazi ya uuguzi katika hospitali ya umma.

11.  Kuchomwa kwa familia ya Ridhaa kunamletea ugojwa wa shinikizo la damu lakini anasaidiwa kudhibiti hali hiikutokana na huduma za ushauri na uelekezaji kutoka kwa wataalamu.

12.  Lime na Mwanaheri wanabakwa lakini wanapata heri abaada ya kutibiwa na wauguzi waliotumwa na mashirika yasiyokuwa ya kiserikali.

13.  Ridhaa anafuraha kupatana na mwanawe Mwangeka vita vya baada ya uchaguzi vilivyozuka na kusababisha wanawe wengine pamoja na mkewe Terry kuangamia.

14.  Usalama unazorota katika nchi ya Wahafidhina lakini wanapata heri jamii ya kimataifa inapowasaidia kurejesha Amani.

15.  Kiriri anamsaidia mfanyikazi wake Kangata kuyadhamini masomo ya binti zake wawili.

16.  Riziki Immaculata, kitoto kinachotupwa na mamake kwenye biwi la taka linapata heri kinapookolewa na Neema anayekipeleka katika kituo cha watoto cha Benefactor.

17.  Umulkeri amekuwa akilia kwa kukosa wazazi lakini hali inakuwa bora kwake Apondi na Mwangeka wanapomchukua na kuishi naye kama mwana wao wa kupanga.

18.  Chanda Chema anataabika kwa kukosa malezi lakini Bwana Tenge na Bi. Kimai wanamchukua na kumlea kama mwanao.

19.  Mwaliko anatekwa nyara na nyumbani kwa Bi.Kangara lakini anaokolewa na polisi na kupelekwa katika kituo cha Benefactor.

20.  Mwangeka anafiwa na mkewe Lily Nyamvula lakini anapata heri anapowoa Apondi.

21.  Apondi anafiwa na mumewe aliyeenda kudumisha amani  lakini anapata nafuu anapoolewa na Mwangeka.

22.  Hazina anataabika barabarani kama ombaomba lakini anapata heri Umu anapompa pesa.

23.  Umulkheri anapoteseka mjini anabahatika kumpata Hazina aliyempa pesa miaka mingi iliyopita. Hazina anamsaidia Umukheri.

24.  Dick anapata heri anapojinasua kutoka kwenye biashara ya kuuza dawa za kulevya na kuanza biashara yake ya kuuza vifaa vya elekroniki.

25.  Tuama anapoteza damu nyingi baada ya kupashwa tohara lakini anapata heri anapotibiwa na kupona.

26.  Neema anataabika kwa kukosa mtoto lakini hali yake inaimarika anapofaulu kupewa Mwaliko na Mtawa Anastacia kutoka kituo cha watoto cha Benefactor na kumlea kama mtoto wa kupanga.

44 comments:

  1. I just came across this blog and to be sincere I love it. Naomba mshughulikie mbinu nyinginezo katika chozi la heri tafadhali.
    Am a kisw/hist. teacher and am raedy and willing to support this blog.

    ReplyDelete
  2. Thank you for the complement. Tunatafiti maswala mengine katika vitabu vya fasihi. Keep revisiting the blog for more updates.

    ReplyDelete
  3. Enter your comment...this blogspot is so good I like it so much asanteni sana

    ReplyDelete
  4. I am glad to have found concrete information on chozi la heri,this is so commendable.kudos to those who does this

    ReplyDelete
    Replies
    1. πŸ€πŸ€πŸ€πŸ‘πŸ‘πŸ‘πŸ’ͺπŸ‘πŸ‘

      Delete
    2. Kuhusu ufaafu Wa Anwani bado sijaelewa kama inazungumziya kuhusu mbinu gani

      Delete
  5. This is excellent big up to all the brains behind this master piece.We hope to get more

    ReplyDelete
  6. Thank you. You encourage us to do even more.

    ReplyDelete
  7. This platform is so good am also using it for revision purpose. Am currently in form three.

    ReplyDelete
  8. I am a candidate. Love your website. Very helpful. Best I've used so far

    ReplyDelete
  9. Thanks gays you have made me to pass kiswahili

    ReplyDelete
  10. Wow 😲 it's made me finish my assignment l don't know what would l have done without it bonjour

    ReplyDelete
  11. This website has been of great help ....... Thanks alot

    ReplyDelete
  12. Kazi maridhawa sanaπŸ‘πŸ‘

    ReplyDelete
  13. Actually me as a student am really helped, thank you for the updates and keep it up

    ReplyDelete
  14. Asante. Sana
    Mwalimu

    ReplyDelete
  15. Thanks for the update

    ReplyDelete
  16. Thanks I loved it ❤️

    ReplyDelete
  17. Mimi ni Antony mwanafunzi wa shule ya upili ya Kiamwangi naomba kuongezwa kwa house za ufaafu wa anwani chozi la heri

    ReplyDelete
  18. I love this very much. it's so detailed keep bringing more of this asaaantee sana🀝🀝

    ReplyDelete
  19. it's just helpful thanks for your updates.....my name is Brian

    ReplyDelete
  20. I appreciate, it's so helpful I learned a lot and for that I can just say thanksπŸ‘πŸ‘πŸ‘

    ReplyDelete
  21. Thnks jmni munatusaidia snaa

    ReplyDelete
  22. Thanks so much 😊

    ReplyDelete
  23. Thanks atleast i have learnt something

    ReplyDelete
  24. Ahsante sana nashukuru kwa kuwa nimefaidikaa sana. Kazi safi kweli.

    ReplyDelete
  25. Nashukuru kwani imenifaidi sanaa kongole

    ReplyDelete

SPECIAL FEATURE-PHOTOSYNTHESIS

  PHOTOSYNTHESIS AND WHY IT IS IMPORTANT Photosynthesis and Why it is Necessary Photosynthesis is a critical process that sustains plants ...