BLOG VISITORS

Thursday, May 14, 2020

NDOA KATIKA CHOZI LA HERI


MAUDHUI YA NDOA KATIKA CHOZI LA HERI
                            
Ndoa ni makubaliano rasmi ya mwanaume na mwanamke kuishi pamoja kama mume na mke. Pia huitwa chuo. Katika riwaya ya Chozi la Heri, maudhi ya ndoa yanajitokeza baina wahusika mbalimbali. Ndoa hizi zinakumbwa na changamoto tofauti tofuti huku zingine zikisambaratika na zingine zikiimarika. Mifano ya ndoa riwayani ni kama yafuatayo:

Ndoa kati ya Mwimo Msubili na wake zake kumi na wawili akiwemo mamake Ridhaa. Ridhaa ni mmoja wa zao la ndoa hili.

Ndoa kati ya Ridhaa na Terry. Wanaozaliwa kutokana na ndoa hii ni Mwangeka, Annatila(Tila) Dede na Mukeli.

Ndoa kati ya Mwangeka na Lily Nyamvula. Becky anazaliwa kutokana na ndoa hii lakini anaangamia katika mkasa wa kuchomwa kwa jumba la Ridhaa. Lily pia anateketea katika mkasa huo.

Ndoa kati ya Racheal Apondi na Mandu. Wanamzaa Sophie. Mandu anaaga vitani anapoenda kulinda Amani ughaibuni.

Ndoa kati ya Mwangeka na Racheal Apondi baada ya wawili hawa kufiwa na wenzao katika ndoa zao za kwanza. Wanamzaa Ridhaa.

Ndoa kati ya Kaizari na Subira. Lime na Mwanaheri ni mazao ya ndoa  hii.

Ndoa kati ya kangata (mfanyikazi wa Kiriri) na Ndarine. Wanawazaa Lunga Kiriri Kangata, Akelo Kiriri-Kaango na Lucia Kiriri Kangata.

Ndoa kati ya Akelo Kiriri na Kaango. Wawili hawa wanawazaa Ngaire na Mumbi.


Ndoa kati ya Kiriri (tajiri aliyemwajiri Kangata) na Annet. Wanawazaa Songoa na wengine walioenda kusomea na baadaye kufanya kazi ughaibuni.

Ndoa kati ya Lunga na Naomi. Wanawazaa Umulkheri, Dick na Mwaliko.

Ndoa kati ya Billy na Sally. Ndia hii inasambaratika kwa sababu Sally anasema kwamba hawezi kuishi katika “nest” ambayo ilijengwa na Billy. Anakataa na kurudi kwa ughaibuni.

Ndoa kati ya Neema na Mwangemi. Wawili hawa wanakosa kupata mtoto na hivyo wanaamua na kumpanga Mwaliko.

Ndoa kati ya Bwana Tenge na Bi. Kimai. Bwana Tenge si mwaminifu katika ndoa hii na hukigeuza chumba chake danguro wakati Bi. Kimai ameenda nyumbani.

Ndoa kati ya mamake Sauna na Bwana Kero. Wanamzaa Sauna.

Ndoa kati ya Bwana Maya na mamake Sauna

Ndoa kati ya Shamsi (Bwana Dengelua) na Bi. Halua ambaye ni mkewe.

Ndoa kati ya Pete na Fungo.

Ndoa kati ya Pete na Nyangumi.





POST A COMMENT DOWN THERE πŸ‘‡

8 comments:

SPECIAL FEATURE-PHOTOSYNTHESIS

  PHOTOSYNTHESIS AND WHY IT IS IMPORTANT Photosynthesis and Why it is Necessary Photosynthesis is a critical process that sustains plants ...