BLOG VISITORS

Saturday, May 23, 2020

UFAAFU WA ANWANI TUMBO LISILOSHIBA


UFAAFU WA ANWANI TUMBO LISILOSHIBA


Tumbo Lisiloshiba ni anwani ya moja kati ya hadithi zilizotungwa na Said A.  Mohamed. Hadithi hii inapatikana katika kitabu cha hadithi fupi chenye jina Tumbo Lisiloshiba na Hadithi Nyingine. Kitabu hiki kimehaririwa na Alifa Chokocho na Dumu Kayanda.

Kichapishi changu hiki kinaegemea hadithi ya kwanza kwenye kitabu hiki ambayo ni Tumbo Lisiloshiba. Utafiti wangu unachunguza ufaafu wa anwani hii katika hadithi hii. Je, anwani hii inaifaa hadithi hii au la? Bila shaka hoja zifuatazo zinadhibitisha kuwa anwani hii inaiafiki hadithi hii.

Viongozi wamejenga majengo mengi mjini na kumaliza nafasi yote hadi hakuna nafasi ya kuvuta pumzi.

Viongozi wana majengo mengi mjini lakini bado wanahitaji ardhi zaidi ya kujengea majengo mengine.

Kutotosheka kwa matajiri kunawafanya kutaka kuwapokonya Wanamadongoporomoka ardhi zao bila kujali kule ambako maskini hao wangeenda.

Viongozi wameweka vikwazo vya kisheria ili raia wasiweze kuzitetea mali zao baada ya wao kuwanyanganya.

Jitu lina tumbo lisiloshiba kwa vile linaingia mkahawani na kula chakula chote kilichokuwa kimepikwa.

Jitu hilo pia linaagiza kuandaliwa chakula maradufu ambalo lingekuja kula mkahawani siku ambayo ingefuata.

Kwasababu ya kutotosheka kwa viongozi, wanawabomolea raia makazi yao wakiwa wamelala ili waweze kuinyakua ardhi zao.

Tamaa ya viongozi inawafanya kuwatumia askari wa baraza la jiji pamoja na jeshi la polisi ili kuwasaidia kupata ardhi zaidi wakati tayari wana majengo mangi mjini.

Wanasheria wamekosa uaminifu kwa sababu ya tamaa ya pesa. Wanakosa kuwatatulia masikini sharia ngumu zinazowakabili.

Viongozi wanataka kuwalipa Wanamadongoporomoka fidia duni/ visenti vichache ili waondoke Madongoporomoka na kuwaachia ardhi hiyo.

Kutokana na hoja hizi, niko radhi kutoa uamuzi kwamba anwani Tumbo Lisiloshiba inaiafiki hadithi hii. Wawezadondoa hoja zingine ambazo zinadhihirisha kwamba ni kweli anwani hii inaifaa hadithi hii.

GUSA HAPA KUPATA WAHUSIKA KATIKA TUMBO LISILOSHIBA


TOA MAONI AU ULIZA SWALI HAPO KWENYE SEHEMU YA COMMENT πŸ‘‡

MAUDHUI TAWALA KATIKA TUMBO LISILOSHIBA

12 comments:

  1. Kwa kurejelea hadithi ya mapenzi ya kifaurongo na shogake dada and ndevu fafanua changamoto zinazowakumba vijana

    ReplyDelete
  2. Taja umuhimu au majukumu ya kila mhusika uliyemtaja

    ReplyDelete
  3. Kwa uchambuzi zaidi, majibu ya maswali na makala mengine, subscribe channel yetu ye YoutTube hapa.

    https://www.youtube.com/channel/UC3EEBQNhW-y6VNg3JgpN76Q

    ReplyDelete
  4. Huku ukirejelea hadithi ya mame bakari eleza matatizo ya wanawake na nafasi zao

    ReplyDelete
  5. I need sifa ama umuhimu za wahusika

    ReplyDelete
  6. Nafurahia this site really helpful to me

    ReplyDelete
  7. Thank you for good guide

    ReplyDelete

SPECIAL FEATURE-PHOTOSYNTHESIS

  PHOTOSYNTHESIS AND WHY IT IS IMPORTANT Photosynthesis and Why it is Necessary Photosynthesis is a critical process that sustains plants ...