BLOG VISITORS

Sunday, April 19, 2020

INSHA---HOJA/MAUDHUI YA MADA MUHIMU ZA INSHA




HOJA/MAUDHUI YA MADA MUHIMU ZA INSHA

CHANGAMOTO ZINAZOKUMBA VIJANA
ü Magonjwa sugu (ukimwi)
ü Dawa za kulevya
ü Ukosefu wa ajira
ü Umaskini uliokithiri
ü Uigaji wa tamaduni za kigeni
ü Athari za utandawazi
ü uchumi kudoroa (Kustaafishwa mapema)
ü Kuibuka kwa lugha ya vijana isiyoeleweka na wavyele wao, basi kukosa maongozi bora.
ü Shinikizo la hirimu (marika)
ü Ujana (Ushababi)
Taja zozote 5 (changamoto na pendekezo la kusuluhisha)

DHULUMA DHIDI YA WANAUME
ü Kupigwa
ü Kufanyizwa kazi nzito za kinyumbani.
ü Kutusiwa/kukashifiwa.
ü Kunyimwa haki za ndoa.
ü Kukejeliwa (wakosapo ajira)
ü Kushurutishwa kutoa pesa zote.
ü Kunyimwa uhuru wa kutoa maoni.
ü Kunyimwa chakula (wafikapo nyumbani kuchelewa/walevi)

HATUA ZINAZOPASWA KUCHUKULIWA ILI KUIMARISHA MATOKEO YA MTIHANI SHULENI MWETU
Mwili uzingatie hoja zifuatazo.
ü Kuimarisha nidhamu
ü Kununua vifaa vya kimsingi k.v vitabu
ü Kuhimiza matumizi ya Kiswahili na kiingerza shuleni
ü Kuhimiza matumizi yafaayo ya wakati
ü Kuhimiza vipindi vyote vya masomo kuhudhuriwa.
ü Kununua makala ya kudurusu
ü Kuhimiza wazazi kuwajibikia majukumu yao
ü Kuhimiza uwajibikaji  wa walimu na wanafunzi
ü Kutoa nasaha na ushauri katika masomo mbalimbali na umuhimu wa elimu kwa jumla.
ü Kuimarisha mahabara na maktaba
Mtahiniwa azingatie pande zote mbili hasara na faida kasha achukue msimamo

UTANDAWAZI UNA HASARA KULIKO FAIDA JADILI:
Hasara za utandawazi
ü Maovu  kuzagaa haraka kote
ü Miigo ya mambo yasiyofaa
ü Maadili kuzorota
ü Uhalifu kuongezeka
ü Matumizi mabaya ya mtandao
ü Wanafunzi kuchanganyikiwa

Faida za utandawazi
ü Kukuza maendeleo
ü Kubadilishana mawazo
ü Kuimarisha biashara za kimataifa
ü Kuimarisha elimu
ü Kuhimiza mataifa na uchunguzi
ü Kuimarisha teknolgia ya habari na mawasiliano
ü Mtahiniwa azingatie hoja zilizo hapo juu.
Hoja nyiongine zikadiriwe ipasavyo

HOJA MUHIMU ZA TAWASIFU
ü Jina la mwandishi
ü Tarehe ya kuzaliwa
ü Mahali alipozaliwa
ü Wazazi wake
ü Motot wa ngapi katika uzawa wake
ü Jinsia yake
ü Alikosoma na wakait aliposima
ü Alichosemea na livyofaulu
ü Taaluma, kazi na tajriba
ü Uraibu wake
ü Uananchama wowote
ü Mafanikio yake maishani/tuzo na vyeit alivyowahi kushinda
ü Pingamizi zozote alizowahi kukumbana nazo maishani
ü Hali yake ya ndoa/familia
ü Warejelewa wake
ü Semina/makongamano ambayo amewahi kuhudhuria
ü Majukumu au mchango wake katika jamii
ü Matarajio yake/azma yake/manifesto yake katika wadhifa wake mpay wa Useneta
ü Anatetea nini zaidi katikak jamii
ü Falsafa/mtazamo wake katika jamii kuhusu maswali mbalimbali

PENDEKEZA NJIA KADHAA ZINAZOWEZA KUTUMIWA KATIKA KUBUNI NAFASI ZA KAZI HAPA NCHINI
ü Upanuzi wa viwanda
ü Kuimarisha uchmi wanachi ili pesa zipatikane za kuwaajiri watu
ü Kuhimiza watu kujiajiri na serikali
ü Kupunguza mishahara mikubwa mikubwa ili pes hizo zitumike kuajiri watu wengine
ü Uimarishaji wa sekta ya elimu ili watu wapewe ujuzi mbalimbali
ü Masomo shulnie yalenge kufnza ubunifu wa kiakzi
ü Serikali itoe ya kigeni yanayotaka kufanya biashara nchini yawekewe sheira kuwa ni lazima yaajiri idaid Fulani ya wenyeji ndipo yaruhusiwe kufanya biashara nchini
ü Kushiriki katika shughuli za jua kali
ü Wafanyikazi wa kgieni watozwe usuhur ziaidi kwa mishahara yao ili kuwazuia kuja kuchukua nafasi za kikazi mabazo zingekuwa za wenyeji
ü Sekta ya michezo iimarishwe

UHALIFU
Aina za uhalifu
ü Wizi wa kimabavu
ü Mapigano ya kikabila
ü Ugaidi
ü Ubakaji
ü Mauaji ya kikatili
ü Udanganyifu katika biashara (bidhaa gushi)
ü Ulanguzi wa dawa za kulevya
ü Ulanguzi wa binadamu

Njia za kukabiliana na uhalifu
ü Kuwasaka na kuwakamata wahalifu
ü Kuimarisha usalama nchini.
ü KuhimizaWananchi kuripoti visa vya uhalifu au watu wanaowashuku kuwa wahalifu.
ü Tume ya ukaguzi na ukadiriaji wa ubora kutekeleza wajibu wake.
ü Walinda usalama kupewa motisha.
ü Kufutwa kazi kwa maafisa wausalama wanaoshirikiana na uhalifu.

MANUFAA YA UHIFADHI WA MAZINGIRA
ü Kuwepo kwa miti – ivutayo mvua
ü Itupayo chakula, dawa n.k.
ü Hutupa mbao za ujenzi.
ü Tabaka la ozoni likihifadhiwa tutakingwa dhidi ya miale ya jua isababishayo kansa ya ngozi n.k.
ü Binadamu atakuwa na afya nzuri kutokana na hewa safi yenye oksijeni.
ü Uhifadhi wa msitu utazuia maporomoko ya ardhi yasababishayo vifo na uharibifu mkubwa.
ü Misitu pia itasaidia kuzuia gharika iletayo maafa.
ü -Wanyama na mimea itakuwa bila matatizo na yatokanayo na kemikali hatari na takataka nyingine.
ü Mito na maziwa yatakuwa na maji safi.

SABABU ZA KUTOFANYA VIZURI  KATIKA MITIHANI YA KITAIFA
ü uhaba wa walimu
ü uchache wa madarasa
ü uhaba wa vitabu/vifaa
ü kutokamilisha silabasi kwa wakati ufaao
ü Msongamano wa wanafunzi madarasani
ü Uzembe miongoni mwa walimu
ü migomo shuleni

MADHARA YANAYOTOKANA NA UFISADI
ü Kuharibika  kwa miundo msingi kwa vile barabara
ü Ufisadi huwafanya watu kukosa kufanya kazi vizuri
ü Wananchi kukata  tama wakati jasho lao hafalidiwi
ü Viwanda kuporomoka
ü Ufisadi umewatajarisha matajiri huku maskini wakidhulumiwa
ü Ufisad umesababisha ukosefu wa amani
ü Ufisadi umeendeleza ajali nyingi barabarani
ü Ufisadi umeendelea ajli nyingi bvarabarani
ü Ufisadi umesababisha ukosefu wa maadili katika jamii . k,m uavyaji wa mimba
ü Elimu umeadhirika kutokana na maafisa wafsadi

TAJA  MAMBO YANAYOCHANGIA VITA VYA UKABILA
Sababu
ü Siasa – vyama vya siasa
ü uchochezi kutoka kwa viongozi
ü Chuki na uhasama baina ya makabila
ü Umaskini
ü Ukosefu wa ajira
ü Vikundi haramu vya vijana k.m mungiki, sungusungu MRC nk
ü Ugaidi
ü Dhuluma za kihistoria
Mapendekezo
ü Wachochezi kuchukuliwa hatua za kisheria
ü Wananchi kuhamasishwa kuhusu umuhimu wa kuishi pamoja kwa amani
ü Serikali na washikadau kushirikiana ili kukabili tatizo la umaskini
ü Kubuni nafasi za ajira kwa vijana
ü Serikali kukabili vikundi haramu na ugaidi vilivyo

NAMNA KATIBA ILIVYOSHINDWA KUTIMIZA MALENGO YAKE KWA WANANCHI
ü Imeongeza gharama ya mishahara ya wabunge na wawakilishi hivyo kuacha mzigo kwa wananchi
ü Wananchi wengi wamesalia katika maisha ya ukata licha ya mabadiliko ya kikatiba
ü Licha ya katiba kubadilika viongozi walisalia wale wale wenye ufisadi, ukosefu wa utu, katili kutojali n.k
ü Haikupendekeza namna ya kutatua matatizo sugu yanayowakumba wanchi k.v ukosefu wa kazi
ü Serikali imetumia fedha nyingi kufanikisha utekelezaji wake badala ya kuunda miundo misingi ya kuboresha maisha
ü Kuwepo kwa viwango tofauti vya uongozi yaani serikali ya kitaifa  na kimajimbo kumezorotesha kasi ya maendeleo
ü Katiba haikupendekeza malipo / ajira ya wafanyakazi wa umma badala yake ikapendekeza tume kupiga msasa mishahara hiyo

JUHUDI ZA KUPUNGUZA AJALI ZA BARABARANI

ü sheria mpya za usafiri - Michuki
ü Mf.mikanda ya usafiri
ü Vithibiti mwendo kutumika.
ü kusitishwa kwa  safari za usiku
ü Idadi ya abiria kuzingatiwa
ü maafisa wa usalama barabarani kuwa chonjo
ü magari mabovu kuondolewa barabarani
ü vyeti vya madereva kuchunguzwa upya
ü maafisa wa usalama barabarani wanaochukua hongo kuchukuliwa hatua za kisheria.

JADILI FAIDA NA HASARA ZA TEKNOLOJIA YA HABARI NA MAWASILIANO
Faida
ü Uchukuzi na mawasiliano ya haraka kama vile katika  ndege, magari moshi yatumiayo stima,mawasiliano ya meme, barua pepe, kipepesi.n.k
ü Elimu kupitia vyombo kama vile runinga, redio,magazeti n.k
ü Katika kilimo kuna mbinu mpya kupitia kwa utafiti wa kisasa.
ü Katika sekta ya afya, kuna uvumbuzi wa madawa ya kisasa n.k
Madhara
ü Uzembe kwa kutumia vyombo vya kisasa, watu wengine hawawezi kujifanyia jambo lolote mitambo inapokwama.
ü Uozo wa kijamii hasa miongoni mwa vijana sababu ya tarakilishi zinazoonyesha mambo yaliyo miiko katika baadhi ya jamii za kiafrika
ü Madhara yanayoambatana na vyombo hivyo kama vile kuharibika macho kutokana na matumizi ya tarakilishi.
ü Madhara ya vyakula vilivyokuzwa kwa kemikali nyingi n.k.
ü Hata  hivyo,yamkini faida ni nyingi kuliko madhara kwa hivyo ni  muhimu kutambuliwe njia za kujikinga na madhara hayo.

JADILI FAIDA NA KASORO ZA LUGHA YA MATANGAZO YA BIASHARA
Faida za matangazo ya biashara (kuunga)
ü Hutufahamisha ni bidhaa gani zinazopatikana.
ü Hutueleza faida za bidhaa fulani.
ü Huzitaja sifa nzuri za bidhaa.
ü Hutumia lugha ya kushawishi.
ü Hurahusisha kazi ya mnunuzi kuchagua bidhaa.
ü Hutuwezesha kulinganisha bidhaa za aina mbalimbali.
ü Huwasaidia wasomaji /watazamaji kuongeza ufahamu.
Kasoro za matangazo
ü Huwakanganya wasikilizaji /wanunuzi.
ü Hayasemi lolote kuhusu ubaya wa bidhaa.
ü Lugha yenyewe hupotosha.Huathiri maisha ya wanajamii kiafya au kitamanduni.
ü Hutumia chuku sana ambayo huweza kuathiri watumiaji wa bidhaa fulani.
CHANGAMOTO ZA SERIKALI ZA UGATUZI
ü Ukosefu wa usawa katika ugawaji wa fedha gatuzi mbalimbali
ü Kutoelewana kwa serikali kuu na serikali ya jimbo/gatuzi
ü Kutoelewa kwa maana ya ugatuzi kwa magavana
ü Kuingiliwa hasa siasa kwa mchakato wa ugatuzi
ü Ukosefu wa mipango katika kutokeleza ugatuzi
ü Ufisadi wa baadhi ya uongozi ( magavana)
ü Ukosefu wa uwezo wa kuttekeleza majukumu ya serikali ya ugatuzi
ü Miundo msingi hafifu nchini
ü Wafanyikazi wa serikali kuu kukosa imani kwa serikali za majimbo
ü Kudhoofika kwa uchumi wa serikali
ü Ukosefu wa wataalamu ( wana taaluma)
ü Kutowajibika kwa viongozi wa gatuzi

SABABU ZA UDANGANYIFU KATIKA MTIHANI NCHINI
Matokeo/yaliyopatikana
ü Maenedeleo ya teknolojia  mfano rukono kurahisisha mawasiliano
ü Mtihani wa kitaifa kuwa ndio kigezo cha maisha ya baaday
ü Ushawishi kutoka kwa wanafunzi na walimu
ü Kuorodheshwa kwa shule bora/ sifa nzuri kwa shule zinazofanya vizuri
ü Kigezo cha kupandishwa madaraka kwa walimu
ü Kutotayarisha wanafunzi vizuri
ü Kutokamilishwa kwa mtaala wa masomo kwa kuwa ni pana
ü Ushindani miongoni mwa wakuu (walimu) wa shule mbali mbali
ü Uoga wa kutimuliwa kutoka shule Fulani
ü Baraza la kufanya mitihani kutokuwa na usalama wa kutosha
ü Tamaa kwa wafanyikazi wa baraza la kufunza mtihani
Mapendekezo
ü Rukono kutoruhusiwa shuleni hasa wakati wa mtihani kwa wanafunzi au watahiniwa na wasimamizi wa mtihani
ü Kutorodheshwa kwa shule pamoja na wanafunzi bora
ü Kukamilisha silabasi kwa wakati ufaao
ü Kuweka usalama wa kutosha kwa mtihani
ü Hatua kali za kisheria kuchukuliwa kwa watakaopatikana na kosa la wizi wa mtitihani
ü Mjia mbadala kutumika katika kutathmini uwezo na sifa za uongozi kwa walimu
ü Kuwaandaa wanafunzi vizuri kabla hawajafanya mtihani
ü Vigezo vingine kutumika katika uteuzi wa viongozi au wafanyi kazi mbalimbali
MANUFAA YA ELIMU BILA MALIPO KATIKA SHULE ZA MSINGI NA ZA UPILI.
Manufaa
ü Idadi ya wanafunzi shuleni imeongezeka
ü Uliopaji na masali ya karo si mzigo kwa wazazi na shuleni
ü Maktaba na mahabara nk zimeweza kuwa na kai zimeongezeka kuwa na vifaa vya kutosha.
ü Nafasi za kazi zimeongezeka kwa shule na taasisi za Elimu nchini.
ü Wafanyikazi wameweza kupata mishahara yao kwa wakati ufaao
ü Dhuluma na ajira kwa watoto imepungua kwa sababu hakuna kisingizio au kuna sheria kali inayowalinda watoto.
Madhara
ü Uhaba wa Elimu
ü Uhaba wa vifaa kwa shule kwa vile serikali imekuwa na mzigo mzito
ü Kiwango cha Elimu kimeshuka
ü Wazazi huzembea na kuachia serikali mzigo mzito wa gharama
ü Kucheleweshwa kwa malipo na serikali na hivyo kusambaratisha shughuli za masomo shuleni
ü Malipo/pesa zinazotolewa ni kidogo ukilinganisha na mahitaji au hali ya uchumi /maisha
VIJANA WANA UWEZO MKUBWA WA KUENDELEZA NCHI ZAO KULIKO WAZEE-JADILI
Swali hili liwe na pande mbili-kuunga na kupinga
Mtahiniwa mwishowe atoe msimamo kutokana na sehemu aliyoipa hoja nyingi (nzito)
Upande unaounga matahiniwa usipungue haja sita
Kuunga
ü Vijana wana uwezo/nguvu za kutosha,wakilinganishwa na wazee
ü Vijana wengi wana uwezo wa kuvumbua mambo yatakoendeleza nchi
ü Wanaweza kukopa na kuiga mambo mapya ambayo yatafanikisha maendeleo
ü Vijana wana uelewa wa teknolojia ya saha
ü Vijana ni wengi kuwaliko wazee
ü Vijana ni wengi ni vijana hivyo basi wana uwezo na nafsi ya kuendeleza nchi
ü Wanajechi wananchihuhitaji vijana walio na nguvu
ü Katika michezo za aina mbalimbali kuna vijana
ü Wengi wa vijana huwa na uvumbuzi na mioyo ya kushiriki kwa biashara.
Kupinga
ü Vijana waaweza kupapia mambo Fulani kutokana na nguvu/haraka waliyonayo katika maisha
ü Vijana wengi wana mapuuza hasa kwa mashauri ya wazee hii ni changamoto kwa kuendeleza maendeleo
ü Katika kuiga/kukopa ,wanaweza kukopa mambo ambayo huyawezi kutumika katika nchi yao
ü Vijana wengi hukimbilia sehemu ambazo zimeendelea kwa sababu ya kutaka kazi rahisi
ü Wengi wa vijana huhofia kuwa waanzilishi wa maendeleo
ü Vijana wengi uhamia nchi zilizoendelea kwa madhumuni ya elimu na kukosa kurudi kwani wanavutiwa na maendeleo na halo nzuri ya masiha kule nje
ü Aghalabu wazee ni wazalendo-hupenda ncho zao kuwaliko vijana
UKIMBIZI NI SUALA KITAIFA NA KIMATAIFA AMBALO  LINA ATHARI NCHINI KENYA.FAFANUA
ü Mfumo wa elimu kusambaratika /wanafunzi kukatizwa masomo
ü Usalama wa wanajamii kusambaratika
ü Huduma za afya kudorora
ü Watoto kuachwa mayatima
ü Utengano wa kifamilia/ndoa nyingi kuvunjika
ü Watu kuishi wakiwa wa woga
ü Njaa kuangezeka/uhaba wa chakula
ü Uharibifu mkubwa wa mali
ü Utegemezi wa misaada/mzigo kwa serikali watu kuishi katika makazi mabaya/makambi /mahema
ü Upweke /ukiwa baada ya kuachwa na jamaa na marafiki
ü Malazi mabaya/msongamano kambini
ü Ukosefu wa siri/faragha
ü Ubakaji /ulawiti
ü Uchumi wananchi kusambaratika
ü Athari z kisaikolojia

CHANGAMOTO ZINAZOWAKABILI  VIRANJA NA MAPENDEKEZO
changamoto
ü Ukosefu wa motisha wa viranja
ü Ukosefu wa demokrasia wakati wa uteuzi wa viranja
ü Viranja kuadhibiwa mbele ya wanafunzi wengine
ü Mkabala usio  mzuri baina ya viranja na walimu
ü Vitisho kutoka kwa wanafunzi shuleni
ü Viranja kuegemea wajibu wao na kudidimia kimasomo
ü Viranja kuafikia uamuzi bila ya ushauri kutoka kwa walimu kuhusu masuala fulani shuleni
ü Ukosefu wa umoja miongoni mwa viranja
Mapendekezo
ü Kubuni kamati inayoshughulikia malalamishi ya wanafunzi
ü Kuwepo semina ya kila mara ya viranja
ü Walimu na washika dau wengine shuleni kuwapa viranja motisha kwa kuwatuza waliowajibika
ü Kuzingatia sheria za wizara ya elimu kuhusu uteuzi na uchaguzi wa viranja\
ü Adhadu kwa viranja kutekelezwa kwa njia isiyo waaibisha
ü Wanafunzi kuruhusiwa kushiriki baraza mara kwa kujadili matatizo yao na kutoa mapendekezo
ü Idara ya ushauri na uelekezaji kuimarishwa shuleni ili kudumisha nidhanmu ya wanafunzi
MATUMIZI MABAYA YA MALI YA UMMA KATIKA MAGATUZI MBALIMBALI NCHINI NA UPENDEKEZE NJIA ZA KUKABILIANA NA TATIZO HILO
Majibu
ü Wawakilishi wa wodi kujilimbikizia marupurupu ya kila aina.
ü Safari za nje ya gatuzi ambazo hazina manufaa yoyote kwa gatuzi.
ü Ununuzi wa vifaa kwa bei ya juu kuliko ilivyo kwenye masoko.
ü Ujenzi wa barabara na nyumba kwa gharama ya juu kutokana na kuwepo kwa ulaghai wakati wa utoaji wa zabuni.
ü Matumizi mabaya ya magari ya umma Kwamfano magavana kuwa na misafara mirefu ya magarinakuandaa karamu zamarakwamara.
ü Wanakandarasi kulipwa kiasi kikubwa cha pesa kuliko inavyopaswa na kuendeleza miradi duni.
ü Huduma za afya kukumbwa na migogoro ya mara kwa mara kwa sababu yahelazasektahiyokutumiwavibayakwingine.
ü Kuajiriwa kwa maafisa pasi na kuzingatia taaluma yao ila ukabila na unasaba.


VIPINDI VYA SINEMA ZA KIMAGHARIBI KWENYE RUNINGA VINA MADHARA MAKUBWA
ü Matumizi ya lugha ya matusi
ü Kuubomoa utamaduni wa Kiafrika na kuupendelea ule wa kigeni.
ü Huhimiza mahusiano ya kimapenzi yasiyofaa
ü Hutoa mafunzo hasi kwa vijana mfano ugomvi, kulipakisasi, ujambazi n.k.
ü Hukuza uvivu – uraibu wa kuzitazama kila wakati.
ü Hutisha/kutia hofu miongoni mwa watazamaji wa umri wa chini.
ü Baadhi huwa na picha chafu kwa mfano watu wakiwa uchi, picha za ngono n.k.
ü Sinema nyingine huhusu vita, ulevi, dawa za kulevya na hivyo kueneza maadili yasiyofaa.
ü Huwa ghali kununua au hata kulipia ili mtu azitazame.
ü Huwatia watu matumaini wasiyo yaafikia. Kwa mfano, mtu kutamani kuhama nchi yake ili kwenda ng’ambo kuishi maisha ya starehe.

KUPATIKANA KWA MAFUTA NCHINI KENYA KUTACHANGIA KIWANGO KIKUBWA KWAMAENDELEO YA NCHI. JADILI.
Kuunga
ü Ujenzi wa miundo msingi kama vile barabara, mitandao ya simu, mabomba ya kusafisha mafuta,n.k. utafanyika ili kuziunganisha sehemu za uzalishaji mafuta na sehemu nyingine za nchi.
ü Huduma za kijamii kama vile elimu, afya, kazi n.k. zitaimarishwa katika sehemu za visiwa vya mafuta.
ü Wenyeji watapata kazi katika viwanda vya mafuta na hivyo kuinua hali ya maisha.
ü Uchumi wa nchi utaweza kuimarika kutokana na mapato ya  mauzo ya mafuta nje ya nchi.
ü Gharama ya maisha itakuwa chini kutokana na bei ya chini ya mafuta. Hali ya maisha itaimarika.
ü Wananchi wataimarika katika nyanja ya ujuzi katika masuala ya uzalishaji wa mafuta.
ü Biashara za aina mbalimbali zitanawiri kutokana na kipato kitakachowawezesha watu kuwa na fedha za kununulia bidhaa na huduma mbalimbali.
Kupinga 
ü Uzalishaji mafuta utachangia uchafuzi wa mazingira.
ü Migogoro itazuka kautokana na ugavi wa mapato kutokana mapato ya mafuta kwa mfano kati ya serikali ya kitaifa na ile ya gatuzi/kaunti.
ü Uwezekano wa aina mbalimbali za ajali zinazotokana na mafuta na hivyo kusababisha maafa na hasara kubwa.
ü Migogoro baina ya jamii mbalimbali kugombania mashamba kwa sababu ya kupatikana kwa mafuta ndani yake.
ü Uzalishaji wa vyakula utapungua kwa sababu ya utegemezi wa mapato ya mafuta.
ü Mtahini ahakiki hoja za mtahiniwa na akubali hoja zozote mwafaka.

UDANGANYIFU KATIKA MTIHANI WA KITAIFA NI TATIZO SUGU. ANDIKA TAARIFA ITAKAYOSOMWA KWA REDIO KUHUSU SULUHISHO LA TATIZO HILI
Suluhisho
·       Wanafunzi walenge kupata alama kulingana na uwezo wao
·       Wazazi wawe na matarajia kulingana na uwezo wao.
·       Mtazamo wa jamii ubadilishwe
·       Wanafunzi na shule  washindane  (zishindane) kulingana na kiwango
·       Mfumo wa elimu ubadilishwe usiegemee sana kupita mtihani pia uangazie vipawa vya wanafunzi
·       Wasimamizi wawe macho wakati wa kusimamia mtihani
·       Hatua kali kuchukuliwa kwa wale watakao juhusisha na udanganyifu (hoja zozote sita)
KATIBA MPYA ITABORESHA MAISHA YA WAKENYA. JADILI
Baadhi ya hoja za kuunga mkono
ü Kuzingatiwa na haki za binadamu
ü Ugavi wa rasilimali utafanywa kwa uwazi
ü Uongozi mzuri na uajibikaji
ü Kuwepo kwa usawa
ü Ugatuzi utaleta maendeleo
ü Kushirikisha wakenya wote katika maendeleo
ü Maswala ya vta baada ya ucahguzi yatotuliwa
ü Idara ya mahakama kuwa kuwa
ü Umoja wa kitaifa
ü Utangamano
ü Utatilia maanani haki za jamii haswa  zile  zinazohisi kutengwa
ü Utaimarisha democrasia
ü Utaimarisha kuhusisha wananchi katika utawala
Baadhi ya hoja za kupinga
ü Ufisadi-ubadhirifu wa pesa
ü Kuvuruga baadhi ya tamaduni  k.m nafasi ya mwanamke
ü Kuendeleza ukabila
ü Baadhi ya maeneo kubaki nyuma kimaendeleo
ü Migogoro kati ya viongozi k.m magavana na maseneta
ü Utata katika kuelewa, kutafsiri  au kufasiri vifungu vya katiba mpya
ü Serikali kuu kutoachilia baadhi ya vitengo vya utekelezaji wa katiba mpya
ü Matumizi mabaya ya mamlaka na viongozi
ü Kuna baadhi ya vipengele vya katiba mpya ambavyo havijatiwa baadhi ya masharti
ü Ushuru utakuwa mwingi kwa wananchi       

BOFYA HAPA KWA 'O' NA 'AMBA' REJESHI
POST A COMMENT DOWN THERE 👇

3 comments:

SPECIAL FEATURE-PHOTOSYNTHESIS

  PHOTOSYNTHESIS AND WHY IT IS IMPORTANT Photosynthesis and Why it is Necessary Photosynthesis is a critical process that sustains plants ...